Share this PostPin ThisShare on TumblrShare on Google PlusEmail This
Ezekiel King Mwenye shati la blue  akiteta jambo na nduguze kabla ya kutolewa hukumu.picha na Rashid Mkwinda wa Fasihi Midia
 Na EmanuelMadafa,Mbeya
MAHAKAMA ya Hakimu Mkazi Mbeya, imemuhukumu kwenda jela miaka saba, Ezekiel King (52) Mwenyekiti wa serikali ya mtaa wa Itiji (Chadema) Jijini hapa na mwenzake Anthon Kavuruge(53) kwa kosa la shambulio la kudhuru mwili.

Akisoma hukumu hiyo Hakimu wa mahakama ya Mkoa wa Mbeya Maria Batulaine alisema kuwa washitakiwa hao kwa pamoja walishtakiwa kwa kosa la kumdhuru mkazi wa Itiji Nicholaus Mwakasinga kwa kumpiga na kumjeruhi kichwani na mkononi.

Amesema kuwa washitakiwa walitenda kosa hilo Octoba 4, 2013 wakiwa katika kilabu cha pombe kilichopo eneo la Itiji ikiwa ni kinyume cha sheria namba 225 sura ya 16 iliyofanyiwa marekebisho mwaka 2002.

Awali akisoma maelezo  ya uchambuzi wake Hakimu Batulaine amesema, mahakama imechambua na kuthibitisha ya kwamba washitakiwa wote kwa pamoja walitenda kosa hilo licha ya kujaribu kuidanganya mahakama.

Amesema,pia ushahidi wa upande wa mashitaka kutoka  hospitali uliweza kuthibitisha majeraha ya vidonda kwenye mwili wa Mwakasinga huku ukiweka bayana ya kwamba  shahidi namba moja upande wa mashitaka hakuwa na matatizo ya akili kama ilivyoelezwa na washitakiwa.

Aidha, kabla ya kutoa hukumu hiyo, Hakimu Batulane alitoa nafasi ya kujitetea kwa washitakiwa ambao wote kwa pamoja waliiomba mahakama kuwapunguzia adhabu kwani familia zao zinawategemea.

Akitoa hukumu hiyo hakimu Batulane, amesema kuwa  mahakama hiyo i imepitia ushahidi wa pande zote mbili na kwamba umeridhika pasipo kuacha mashaka hivyo kuwahukumu kwenda jela washitakiwa miaka sabana kwamba rufaa ipo wazi.

Hata hivyo Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) John Mwambigija alisema uongozi umepokea hukumu hiyo kwa mshangao mkubwa.

Aidha, amesema tayari uongozi umekutana na kwamba taratibu za kuwasiliana na  mwanasheria wa chama zinafanika ikiwa na kuangalia uwezekano wa kukata Rufaa kabla ya siku 30 kumalizika.
Mwisho.



Je, Una Habari,Picha,Tangazo,Makala, Ushauri n.k.?Basi Wasiliana Nasi Simu/WhatsApp 0759 406 070

Post a Comment

 
Top