Na Bonaface Wambura,Dar es salaam
Mechi ya michuano ya
Afrika kati ya Tanzania (Taifa Stars) na Msumbiji (Mambas) iliyochezwa juzi
(Julai 20 mwaka huu) imeingiza sh. 158,350,000 kutokana na washabiki 19,684
walioingia kwa kiingilio cha sh. 7,000 na sh. 30,000.
Mgawo wa mapato hayo
ulikuwa kama ifuatavyo; Kodi ya Ongezeko la Thamani (VAT) sh. 24,155,084.75,
gharama za tiketi (MaxMalipo) sh. 19,684,000, gharama za mchezo sh. 22,902,183,
uwanja sh. 11,451,092, Shirikisho la Mpira wa Miguu Afrika (CAF) sh. 5,725,546
na Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) sh. 74,432,095.
Tunawashukuru washabiki
wote waliojitokeza kwenye Uwanja wa Taifa kuishangilia Taifa Stars katika mechi
hiyo iliyomalizika kwa sare ya mabao 2-2.
Hata hivyo mara baada ya
Taifa Stars kumalizi kibarua hicho kinatarajia
kuondoka keshokutwa (Julai 24 mwaka huu) kwenda Mbeya ambapo kitapiga kambi ya
wiki moja kujiandaa kwa mechi ya marudiano dhidi ya Msumbiji.
Mechi hiyo ya raundi ya
pili ya michuano ya Afrika kutafuta tiketi ya kushiriki Fainali za Afrika
(AFCON) zitakazochezwa mwakani nchini Morocco itafanyika wikiendi ya Agosti 2
na 3 mwaka huu nchini Msumbiji.
Taifa Stars
inayodhaminiwa na Kilimanjaro Premium Lager itaondoka nchini Julai 31 mwaka huu
kwenda Johannesburg, Afrika Kusini ambapo itafanya mazoezi ya mwisho kabla ya
kutua Maputo kwa ajili ya mechi hiyo itakayochezwa Uwanja wa Taifa wa Zimpeto.
mwisho
Post a Comment