Na Boniface Wambura,Dar es salaam
Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) limeongeza muda wa
usajili kwa wiki mbili ili kuzipa klabu nafasi ya kukamilisha taratibu
zinazotakiwa. Hivyo hatua ya kwanza ya usajili inakamilika Agosti 17 mwaka huu
badala ya Agosti 3 ya awali.
Kutokana na marekebisho hayo, kipindi cha
uhamisho kinakamilika Agosti 17 mwaka huu wakati pingamizi itakuwa kati ya
Agosti 19 hadi 26 mwaka huu.
Kamati ya Sheria na Hadhi za Wachezaji
itathibitisha usajili kati ya Septemba 1 na 2 mwaka huu.
Uhamisho wa kimataifa, usajili wa
wachezaji huru, na utatuzi wa dosari za usajili unatakiwa uwe umekamilika
kufikia Septemba 7 mwaka huu. Uthibitisho wa hatua ya mwisho ya usajili
utafanywa Septemba 15 mwaka huu.
Kwa upande wa Ligi Kuu ya Vodacom (VPL)
msimu wa 2014/2015 itaanza Septemba 20 mwaka huu, na ratiba itatolewa mwezi
mmoja kabla ya kuanza ligi hiyo.
mwisho
Post a Comment