MKURUGENZI wa RJ Company, Vincent Kigosi ‘Ray’ ameshindwa kumzika baba
mdogo wa mkurugenzi
mwenza wa kampuni hiyo, Blandina Chagula, Clement Kiyenze Chagula.
Mzee huyo alifariki katika Hospitali ya Muhimbili kutokana na
matatizo ya presha na figo yaliyokuwa yakimsumbua na kuzikwa katika Makaburi ya
Kinondoni jijini Dar ambapo wasanii mbalimbali wa filamu nchini walishiriki
akiwemo Mbunge wa Chalinze, Ridhiwani Kikwete.
Alipoulizwa Ray kwa nini hakuhudhuria mazishi hayo, alisema:
“Ukweli ni kwamba mimi sipo Dar. Ndiyo maana sijaonekana huko
kwenye mazishi, nipo Mwanza katika shughuli zangu za kikazi, tuko pamoja
lakini,” alisema Ray ingawa wachungzi wa mambo wanasema kuwa alikuwepo mjini
ila ni kutokana na sababu binafsi zao kati yake na Johari ndo maana hakutaka
kwenda huku chuchu hans akidaiwa kuhusika.
Post a Comment