Share this PostPin ThisShare on TumblrShare on Google PlusEmail This


Majirani wakilia kwa uchungu


Mke wa Marehemu akiwa chini baada ya kushudia mwli wa marehemu mumewe ambaye ameachwa na watoto watatu..
 Na Mwandishi wetu,Mbeya
Katika hali isiyokuwa ya kawaida Mkazi wa eneo la Mama John Mtaa wa Kagera jijini Mbeya ambaye jina lake halijafahamika mara moja maarufu (Malebo)  Dereva wa Daladala (34) amekutwa amejinyonga hadi kufa ndani ya nyumba ya mpenzi wake (Mchepuko)  Octoba 31 mwaka huu .

Tukio hilo la aina yake limetokea majira ya saa 7 jioni katika eneo la Mama John jijini hapa ambapo inadaiwa kuwa chanzo cha tukio hilo ni wivu wa mapenzi kwani marehemu huyo  ilikwenda kwa mpenzi wake (Mchepuko)na kukuta nyumba ikiwa wazi bila kuwa na dalili za kuwa na mtu ambapo mara baada ya kuuliza majira alielezwa kuwa mwanamke huyo hakuonekana nyumbani hapo kwa usiku mzima nakwamba hakulala kwakwe.

Aidha baada ya kupata majibu hayo mwanaume huyo aliondoka na kwenda kwa marafiki zake sehemu wanayouzia pombe za kienyeji maarufu (Vamponji) na kuomba ushauri juu ya nini afanye ili kukabiliana na hali hiyo.

Alidaiwa kuwa mwanaume huyo wakati akiomba ushauri alieleza kuwa mpenzi wake huyo ambaye alijulikana kwa majina ya Rebeka Dankeli maarufu Mama Chausiku  alihisi amekwenda kulala kwa mwanaume mwingine kwani wamekuwa wakigombana kw amuda mrefu juu ya kuwepo kwa hali hiyo.

Wakati akitoa malalamiko hayo kwa marafiki zake alielezwa kuwa nivema mambo hayo wakayamaliza wenyewe kwani imekuwa kero kwao hasa kutokana na kwamba wamekuwa wakigombana mara kwa mara na kushulishwa na majirani hao hivyo wamechoka na kwamba aondoke na akayamalize yeye mwenyewe.

Kutokana na hali hiyo mwanaume huyo aliondoka katika eneo hilo la kuuzia pombe za kienyeji iliopokwenda kupata ushauri na kurudi katika nyumba anapoishi hawala yake huyo huku akiendelea kutafakari yale yanayomsibu katika moyo wake pamoja na kuangalia kama mwanamke huyo atarudi au laa.

Baada ya kukaa kwa muda mrefu pasipo kumona mpenzi wake ambapo ilikuwa imefika majira ya saa mbili kasoro aliamua kuchukua maamuzi ya kukatisha uhai wake kwa kujinyonga.
Akizungumzia hali hiyo Mwenyekiti wa Mtaa  huo Ndugu Anyokisye Mwambona amesema tukio hilo la kujinyonga kwa mwanaume huyo nilakwanza kutokea katika maeneo hayo.

Amesema taarifa za kujinyonga alizipata majira ya saa mbili kasoro ambapo alichukua jukumu la kutoa taarifa kwa jeshi la polisi kwa lengo kutoa mwili wa marehemu huyo ndani ya nyumba hiyo.

Kwa mujibu wa mwenyekiti huyo anasema mwanaume huyo tayari alikuwa na mke wake na alikuwa na watoto watatu hivyo tukio hilo limetokea kwa nyumba ndogo (Mchepuko) nakwamba kesi juu ya mwanaume huyo amekuwa akizipata mara kwa mara hivyo  hatua ya mwanaume huyo kujinyonga inawezekana ikawa ni wivu wa mapenzi.

 Amesema tuko hilo liliteka hisia za wakazi wengi wa eneo hiloo kwani mwanaume huyo alikuwa na familia yake hivyo maamuzi aliyoyachukua ni makubwa na yataigharimu familia yake kwa kiasi kikubwa hasa kutokana na watoto wenye kuwa na umri mdogo pamoja na mke wake kutokuwa na shughuli yoyote.

Vilio na majonzi yalitawala baada ya mke wa marehemu huyo halali alipofika katika eneo hilo la tukio na kuanza kulia kwa sauti kubwa huku akitamka maneno ambayo yaliwaliza wengi walitokea katika tukio hilo.

Alidai kuwa amekuwa akimkanya mumewe huyo kwa muda mrfu juu ya kuachana na mwanamke huyo lakini amekuwa hasikii hivyo yaliyokumkuta ni ukaidi wake alieleza mama huyo huku akitazama  mwili wa mumewe ukuwa juu uneninginia .

Hata hiyo Kamanda wa polisi Mkoani hapa Ndugu Ahmed Msangi  amethibitisha kutokea kwa tukio hilo ambapo mwili wa marehemu umehifadhiwa katika hospital ya rufaa mbeya.
Mwisho.


Je, Una Habari,Picha,Tangazo,Makala, Ushauri n.k.?Basi Wasiliana Nasi Simu/WhatsApp 0759 406 070

Post a Comment

 
Top