Share this PostPin ThisShare on TumblrShare on Google PlusEmail This
Staa wa Bongo Movies , Salma Jabu ‘Nisha’ amedai kuwa ana kazi kubwa katika kulinda nafasi yake ya uigizaji bora wa Komedi na ustadi katika kutengeneza kazi zake na ziendelee kuwa bora ili asipotee na kuonekana kama alibahatisha.
Wahenga husema kuwa ni rahisi kupata nafasi ya kwanza, lakini si rahisi kuilinda hivyo name lazima niilinde nafasi yangu niliyoipata mwaka jana baada ya kuipigania kwa muda mrefu katika tasnia ya filamu na nitailinda kwa kufanya kazi bora tu,”anasema Nisha.
Msanii huyo anaamini kuwa kwa Bongo si kazi nyepesi kufanya kazi na kukubalika na wapenzi wa filamu kwani kila siku wasanii wanaongezeka na kuja katika hali ya ushindani mkubwa ambao kama haujajipanga lazima upotee katika tasnia ya filamu baada ya kuvuma kwa muda mfupi tu.

Je, Una Habari,Picha,Tangazo,Makala, Ushauri n.k.?Basi Wasiliana Nasi Simu/WhatsApp 0759 406 070

Post a Comment

 
Top