Share this PostPin ThisShare on TumblrShare on Google PlusEmail This
Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akihutubia vijana wa boda boda ,Stendi Kuu kata ya Mawenzi ambapo aliwaambia kuwa boda boda ni sehemu ya kupata kipato hivyo inabidi wafanye shughuli yao hiyo kwa umakini mkubwa ,ikiwa kudumisha umoja, kufuata sheria, kujisajiri na kutambulika na mamlaka husika ,kuaminika ili waweze kukopesheka.
Katibu wa Umoja wa Boda Boda Moshi mjini akisoma risala kwa Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana kwenye mkutano uliofanyika ,Stendi Kuu kata ya Mawenzi Moshi mjini.
Wafanyabiashara wa soko la kati,Moshi mjini wakiwa wamefunga njia kuzuia msafara wa Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana usipite mpaka wawasilishe kero yao ya kufungiwa soko kwa mwaka mzima na uongozi wa halmashauri ya mji kwa maelezo ya kupisha ukarabati ambao haujafanyika.
Katibu wa Itikadi na Uenezi Nape Nnauye akisoma ujumbe ulioandikwa kwenye mabango na wafanyabiashara wa soko la kati,Moshi mjini.
Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akisoma risala ya wafanyabiashara wa soko la kati,Moshi mjini.
Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akizungumza na wafanya biashara ambao soko lao limefungwa kwa zaidi ya mwaka mmoja sasa.
Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akiongozana na Katibu wa NEC Itikadi na Uenezi Nape Nnauye kuingia kwenye soko la kati, Moshi mjini mkoani Kilimanjaro ambalo lilifungwa kupisha ukarabati ambao mpaka sasa ni mwaka 1 hakuna kilichofanyika na wafanyabiashara wanaishi maisha magumu.
Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akiongozana na Katibu wa NEC Itikadi na Uenezi Nape Nnauye kuingia kwenye soko la kati, Moshi mjini mkoani Kilimanjaro ambalo lilifungwa kupisha ukarabati ambao mpaka sasa ni mwaka 1 hakuna kilichofanyika na wafanyabiashara wanaishi maisha magumu.
Katibu wa Vikoba kata ya Kongoroni Mariam Chawapoma akisoma risala ya kikundi chao kwa Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana
Wanachama wa Vikoba wakishangilia jambo wakati wa mkutano na Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana
Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akihutubia wanachama wa Vikoba kata ya Makongoroni ambapo alishiriki kuzindua vikoba 11 vyenye wanachama 330,Kata ya Makongoroni,Moshi mjini.
Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akishiriki kufyatua matofali baada ya kutembelea kikundi Vijana cha Kata ya Miembeni
Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akipokelewa na umati wa akina mama Lishe wa Njoro,Moshi mjini.


Je, Una Habari,Picha,Tangazo,Makala, Ushauri n.k.?Basi Wasiliana Nasi Simu/WhatsApp 0759 406 070

Post a Comment

 
Top