Waziri mkuu wa Uingereza David
Cameron amewasilisha hoja zake leo akisisitiza umuhimu kuhusu ni kwa
nini Uingereza inapaswa kujiunga na muungano wa mataifa yanayofanya
mashambulio ya angani dhidi ya Islamic State nchini Syria.
Akihutubia
bunge la nchi hiyo amesema haieleweki kwamba Uingereza ingali
inasitasita na kutarajia mataifa mengine yabebe mzigo wa kupigana na
Islamic State pekee yao ilhali tishio la ugaidi unakabili ulimwengu
mzima,Uingereza ikiwemo.
Bw. Cameron ameuliza hata baada ya
mashambulio ya Ufaransa ikiwa Uingereza haitachukua hatua yoyote
washirika wetu wataiuliza kama sasa sio wakati mwafaka basi ni lini ?
Hata
hivyo baadhi ya wapinzani wamehoji ikiwa mashambulio kama hayo
yatapunguza au kuongeza vitisho vya Uingereza kulengwa na kundi hilo.
Kiongozi wa chama cha leba , Jeremy Corbyn,ameuliza msururu ya maswali kuhusu mpango huo
"Hamna
shaka kwamba IS ni tisho hata kwetu ssi Uingereza lakini swali ni je
tukielekeza mashambulio yetu Syria hilo ndilo litapunguza au kuongeza
tisho la Uingereza kushambuliwa.''
'' je hiyo ndio njia mwafaka ya kukabiliana na Islamic State au itasambaza itikadi kali ya ISIL huko mashariki ya kati?."
Mapema
mwezi huu kamati inayohusika na masuala ya kimataifa nchini Uingereza
ilisema kuwa hatua za kijeshi za Uingereza nchini Syria haziwezi
kufanyika bila ya kuwepo mikakati mizuri ya kulishinda kundi la .CHANZO BBC
Post a Comment