Rais wa Marekani Barack Obama
amesema bintiye wa miaka 15, Sasha, alimcheka kwenye ujumbe aliowatumia
marafiki zake kupitia mtandao wa kijamii wa Snapchat.
Kiongozi
huyo wa Marekani amesema Sasha alimpiga video akijadili mtandao huo wa
kijamii kwenye dhifa ya familia na kisha, kisiri akawatumia marafiki
zake akiwa ametoa maoni yake.
Hii si mara ya kwanza kwa rais huyo kujadili shughuli za mtandaoni za bintiye huyo.
Mwezi
Julai, alisema kwamba Sasha hutumia Twitter na kusababisha baadhi ya
vyombo vya habari kujaribu kutambua akaunti ya Sasha kwenye Twitter. |
Post a Comment