Share this PostPin ThisShare on TumblrShare on Google PlusEmail This
ULI
Mshambuliaji wa TP Mazembe na timu ya Tanzania ‘Taifa Stars’  Thomas Ulimwengu  amejiunga  na  timu ya Ligi Daraja la Kwanza Nchini Sweden inaitwa Athletic Football Club Eskilstuna kwa mkataba miaka miwili
 
Baada ya mkataba wake ulimalizika, Mabingwa wa kombe la Shirikisho barani Afrika TP Mazembe Ulimwengu  hakutaka kuongeza mkataba mwingine kwani mawazo yake yalikuwa ni kumfuata rafiki yake Mbwana Samatta anayekipiga KRC Genk ya Ubelgiji .
 
Akizungumza na  Ulimwengu alisema: “Kweli nimesajiliwa kwa mkataba wa miaka miwili kuitumikia timu hiyo ambacho nitajiunga nayo hivi karibuni.
 
“Kwa sasa nashughulikia mambo ya visa kuanzia wiki ijayo  nitaenda nimeshajiunga na timu ya Athletic Football Club Eskilstuna  ya Sweden.”
 
Ligi hiyo ya daraja la Kwanza inashirikisha timu kumi na nne na inatarajia kutumia vumbi April kumi na nne mwaka huu.

Je, Una Habari,Picha,Tangazo,Makala, Ushauri n.k.?Basi Wasiliana Nasi Simu/WhatsApp 0759 406 070

Post a Comment

 
Top