Mwanamke ambaye alishambuliwa na
mmewe na kukatwa mikono nchini Kenya, baada ya ndoa yao kuvunjika kwa
kishindwa kuzaa mtoto, sasa anaripotiwa kuwa mjamzito.
Muda mfupi
baada ya kushambuliwa, Jackline Mwende alisema kuwa madaktari walikuwa
wamewajulisha kuwa yeye alikuwa na uwezo wa kushika mimba, lakini mmewe
Stephen Ngila, hakuwa na uwezo wa kuzaa.
Kwenye mahojiano na gazeti na Daily Nation, Mwende amesema kuwa hali hii ilichangia aanze uhusiano mwingine.
Anasema
alikuwa na haja ya kuwa na watoto ndipo akaanza uhusiano na mwanamume
mwingine ili kuokoa ndoa yake, lakini mumewe ambaye sasa anakabiliwa na
kesi ya kutaka kuua akagundua.
"Nilikuwa ninataka mtoto. Nilikuwa
na haja ya mtoto...na pia ibilisi alisababisha mimi kutembea nje ya ndoa
yangu. Haikuwa vizuri kufanya hivyo, ninajua watu watanihukumu vikali
kwa sababu ya hilo. Kwa vile niko hai na nitajifungua mtoto hivi
karibuni, nini matumaini licha ya kupitia taabu." Alisema mwende.BBC |
Post a Comment