Share this PostPin ThisShare on TumblrShare on Google PlusEmail This
mwakyembe
Waziri mpya wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Dk Harrison Mwakyembe amewataka wanamichezo kumpa ushirikiano katika kuendeleza gurudumu la maendeleo.
Dk Mwakyembe ambaye amechukua nafasi ya Nape Nnauye amesema anaweza kufanya vizuri kama watashirikiana pamoja na wadau wa michezo.
“Tukishirikiana kila jambo litaenda vizuri, serikali inataka mabadiliko, inataka mafanikio na hii ni kwa faida ya wanamichezo. Tushirikiane,” alisema.
Jana, Dk Mwakyembe alikaa kikao cha kwanza cha Kamati ya Serengeti Boys na baadaye akaenda Uwanja wa Taifa kuiunga mkono Taifa Stars iliyokuwa inacheza mechi ya kirafiki dhidi ya Botswana na kuibuka na ushindi wa mabao 2-0, yote yakifungwa na nahodha Mbwana Samatta.

Je, Una Habari,Picha,Tangazo,Makala, Ushauri n.k.?Basi Wasiliana Nasi Simu/WhatsApp 0759 406 070

Post a Comment

 
Top