Mkuu wa mkoa wa Singida Dkt.
Rehema Nchimbi akipata maelezo katika chumba cha kujifungulia akina mama
wajawazito katika zahanati ya kijiji cha Mwahango iliyojengwa kupitia
TASAF 111 na ushiriki wa wananchi wa kijiji hicho mara baada ya
kuizindua.
Mkuu wa mkoa wa Singida Dkt.
Rehema Nchimbi akipima uzito katika zahanati ya kijiji cha Mwahango
iliyojengwa kupitia TASAF 111 na ushiriki wa wananchi wa kijiji hicho
mara baada ya kuizindua.
Mratibu TASAF Mkoa wa Singida
Patrick Girigo Kasango akito taarifa ya Mkoa ya Miradi ya TASAF katika
hafla ya uzinduzi wa zahanati hiyo iliyojengwa kwa msaada wa TASAF 111
na wananchi wa kijiji hicho.
Mkuu wa Mkoa wa Singida Dkt.
Rehema Nchimbi akizindua jengo la zahanati ya kijiji cha Mwahango
iliyojengwa na TASAF 111 na ushiriki wa wananchi wa kijiji hicho
kilichopo wilaya ya Singida, kushoto kwake ni Mwenyekiti wa Halmashauri
ya Wilaya ya Singida Eliya Digha.
Jengo la zahanati ya Mwahango
lililopo halmasahuri ya wilaya ya Singida iliyojengwa kwa msaada wa
TASAF 111 na wananchi wa kijiji hicho.MAELEZO YA PICHA:
……………………….
Mfuko wa maendeleo ya jamii
(TASAF) Mkoa wa Singida umetumia zaidi ya shilingi milioni 430.3 kwa
ajili ya kugharamia ujenzi wa zahanati nne katika halmashauri za wilaya
ya Ikungi, Mkalama, Singida vijijini na Manispaa ya Singida.
Fedha hizo pia zimegharamia
ujenzi wa nyumba mbili (two in one) za kuishi walimu katika shule ya
msingi Chikombo wilaya ya Manyoni na shule ya Msansao iliyopo wilaya ya
Iramba.
Ujenzi wa miundombinu hiyo
kupitia TASAF 111 kipengele cha ujenzi wa miundombinu maalumu umefanyika
kati ya Septemba 2014 na machi mwaka huu.
Hayo yamesemwa jana na mratibu
wa TASAF mkoa wa Singida Patrick Kasango wakati akitoa taarifa yake ya
utekelezaji wa ujenzi wa zahanati ya kijiji cha Mwahango kata ya
Ilongero halmashauri ya wilaya ya Singida.
Amesema wananchi wa vijiji
ambapo miradi hiyo inatekelezwa wamechangia zaidi ya shilingi milioni
61.6 kwa kuchangia nguvu zao kwa kusomba michanga, maji na kuchimba
msingi wa majengo hayo.
Kasango amesema kabla ya
utekelezaji wa miradi hiyo kulifanyika tathimini na uhakiki ili kubaini
hali halisi ya uhitaji wa huduma halisi.
“Pia lengo ni kujiridhisha
kwamba miradi hiyo kama itaweza kusaidia walengwa kutimiza masharti ya
elimu bora na afya katika mpango wa kunusuru kaya maskini, katika
halmashauri sita mkoani kwetu”, amesema.
Kasango ameongeza kuwa kati ya
septemba 2014 hadi machi mwaka huu TASAF 111 Mkoa wa Singida imetumia
fedha zingine zaidi ya shilingi bilioni 23.1 kugharamia utekelezaji wa
kipengele cha uhawilisha fedha (conditional cash Transfer) ambapo kaya
38,984 za vijiji 277 kutoka halmashauri sita zimenufaika na fedha hizo.
Aidha amesema katika programu
ya kutoa ajira za muda kwa kaya maskini, zaidi ya shilingi bilioni 2.7
zimelipwa kwa kaya zilizofanya kazi za muda, ikiwemo ujenzi wa mabwawa
ya maji, na upandaji miti.
Kwa upande wake Mgeni rasmi
katika hafla ya uzinduzi wa Zahanati ya Mwahango Mkuu wa Mkoa wa Singida
Dkt. Rehema Nchimbi ametumia fursa hiyo kuuomba uongozi wa mfuko wa
maendeleo ya jamii (TASAF) makao makuu kusaidia ujenzi wa nyumba kubwa
(two in one) katika zahanati hiyo.
“Binafsi na kwa niaba ya
wananchi wa Mkoa wa Singida naishukru sana TASAF 111 kwa kufanya mambo
makubwa na umekuwa mkombozi kwa wananchi kiuchumi. Mkurungezi TASAF
makao mkuu usichoke kutusaidia, wananchi wa kijiji cha Mwahango wapo
tayari kushiriki ujenzi wa nyumba ya watumishi, na wewe nakuomba uwaunge
mkono kadri uwezo utakapokuruhusu”, amesema Dkt. Nchimbi.
Dkt. Nchimbi ameongeza kuwa
wananchi wa Mwahando wanapaswa kuitunza zahanati hiyo kwa kutumia huduma
zinazopatikana hapo ili manufaa yake yaonekane pia waitunze kwa kupanda
miti eneo la zahanati ili kutunza mazingira.
Aidha ameahidi pikipiki
itakayosaidia utoaji wa huduma katika zahanati hiyo huku akitoa shilingi
laki tano ili ujenzi wa nyumba ya watumishi wa zahanati uanze mara moja
na kuwezesha zahanati hiyo kutoa huduma kwa masaa 24.
Awali Afisa Mtendaji wa kijiji
cha Mwahango Leonard Muna amesema jumla ya wakazi 2,776 wa kijiji hicho
watanufaika na huduma za afya zitakazotolewa kwenye zahanati hiyo mpya.
“Kukamilika kwa zahanati
kutasaidia wanakijiji kupata huduma za kiafya kwa karibu zaidi na hasa
akina mama na watoto. Pia mradi utasaidia kuinua uchumi/kipato cha
wanajamii kwa vile kupunguza muda wa kufuata huduma za afya na kupata
muda mrefu wa kuzalisha huku afya zikiimarika ”, amesema Muna.
Amesema hapo awali wananchi
wamekuwa wakifuata huduma za afya katika zahanati ya Ilongero zaidi ya
kilomita tano ambapo shida kubwa walikuwa wakiipata hasa kwa kuwapeleka
wajawazito kwa kuwabeba kwenye vitanda na mikokoteni kutokana na
kukosekana kwa usafiri wa uhakika kijijini hapo.
Post a Comment