Mwanamke mmoja amefariki akipiga picha aina ya Selfie na rafikiye katika barabara ya treni nchini Thailand.Rafikiye
alisema kuwa walikuwa wamekunywa pombe na kuamua kujipiga picha hiyo na
treni lakini hawakuona treni nyengine iliokuwa ikija kutoka barabara
nyengine ya treni, kwa mujibu wa polisi.
Miguu yake ilikatika na kufariki hospitalini ambako alikuwa amepelekwa kwa matibabu zaidi.
Rafikiye wa kiume alipata majeraha mabaya.
Idadi ya watu wanaofariki wakipiga selfie katika maeneo hatari inaongezeka.
Kisa
hicho kilitokea siku ya Alhamisi asubuhi katika kituo cha treni cha
Samsen mjini Bangkok, kulingana na maafisa wa polisi wa Wissanusak Seub
akiongezea kwamba maafisa walikuwa wakichunguza kilichotokea |
Post a Comment