KESI
ya matumizi mabaya ya madaraka inayomkabili aliyekuwa Mkurugenzi mkuu wa
zamani wa Shirika la Utangazaji Tanzania (TBC), Tido Mhando kuanza
kusikilizwa Machi 28, mwaka huu
Hatua hiyo inakuja baada ya mtuhumiwa huyo leo Februari 28, kusomewa maelezo ya awali (PH), Katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu mbele ya Hakimu Mkazi Mfawidhi, Victoria Nongwa
Kabla ya kusomewa PH, Mhando alikumbushwa mashtaka yake yanayomkabili na Wakili wa Serikali Dismas Mganyizi.Katika
maelezo hayo ya awali, Tido amekubali maelezo yake binafsi ya kwamba
alikuwa Mkurugenzi Mkuu wa TBC mwaka 2006 hadi 2010 na kuwa alikuwa
msimamizi katika shughuli za TBC lakini siyo kwa shughuli zote.
Pia
alikubali kutoa maelezo katika Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa
(Takukuru) lakini hakukiri na kuwa alifikishwa mahakamani Januari
26,mwaka 2018.Aidha
Mhando alikana mashtaka yote yanayomkabili na ksi hiyo itaanza
kusikilizwa kwa upande wa mashtaka kuketa mashahidi wao Machi 28,mwaka
2018.
Mhando anakabiliwa na mashtaka manne ya kutumia madaraka vibaya na moja la kuisababishia Serikali hasara ya Sh.milioni 887.1.
Inadaiwa
kuwa Juni 16,mwaka 2008 akiwa Dubai, Umoja wa Falme za Kiarabu (UAE),
Mhando ambaye alikuwa Mkurugenzi wa TBC, kwa makusudi alitumia madaraka
yake vibaya kwa kusaini mkataba wa kuendesha na utangazaji wa vipindi
vya televisheni kati ya TBC na Channel 2 Group Corporation (BV1) bila ya
kupitisha zabuni, kitu ambacho ni kinyume na Sheria ya Manunuzi na
kuinufaisha BVl.
Katika
shtaka la pili, Mhando anadaiwa kutumia vibaya madaraka yake Juni
20,mwaka 2008 aliposaini makubaliano kwa utangazaji wa digitali duniani
kati ya TBC na BVl.
Katika
shtaka la tatu, anadaiwa Agosti 11,mwaka 2008 na Septemba 2008 akiwa
Dubai, Mhando alitumia vibaya madaraka yake kusaini mkataba wa
makubaliano kwa ununuzi, usambazaji kufunga vifaa vya usambazaji na
mnara wa utangazaji kati ya TBC na BVI na kuifaidisha BVI.
Katika
shtaka la nne, anadaiwa kuwa Novemba 16, mwaka 2008 akiwa Dubai,
Mhando alitumia vibaya madaraka yake kusaini mkataba wa makubaliano kwa
kuendesha miundombinu ya utangazaji (DTT Broadcast Infrastructure) kati
ya TBC na BVI na kuinufaisha BVI.
Katika
shtaka la mwisho, anadaiwa kuwa kati ya Juni 16 na Novemba 16,mwaka
2008 akiwa UAE, Mhando aliisababishia TBCli hasara ya Sh.887,122,219.19.
Post a Comment