Mgodi
wa dhahabu wa Acacia Buzwagi umezindua maktaba iliyogharimu shilingi
milioni 22.4 kwenye shule ya sekondari Bugisha iliyopo katika kata ya
Mondo wilayani Kahama mkoani Shinyanga kwa lengo la kusaidia wanafunzi
na walimu kuchangia katika kuboresha ubora wa elimu inayotolewa.
Maktaba
hiyo imezinduliwa leo Alhamis Februari 8,2018 na Mkurugenzi wa
halmashauri ya Mji wa Kahama,Underson Msumba na kuhudhuriwa pia na
Meneja Mkuu wa Migodi ya Buzwagi na Bulyanhulu,Benedict Busunzu.
Hii ni
maktaba ya pili katika wilaya ya Kahama kuzinduliwa na mgodi huo ambapo
mwaka 2017 mgodi wa Buzwagi ulianzisha maktaba ya jamii katika kata ya
Kagongwa ili kutoa rasilimali za elimu ya aina mbalimbali kwa wanafunzi
na jamii kwa ujumla.
Akizungumza
wakati uzinduzi huo, Meneja Mkuu wa Migodi ya Buzwagi na
Bulyanhulu,Benedict Busunzu maktaba hiyo itasaidia kuboresha upatikanaji
wa elimu kwa wanafunzi kutoka jamii inayouzunguka mgodi wa Buzwagi.
Alisema
kupitia mpango wa Acacia wa maendeleo ya jamii wameamua kushirikiana na
shirika la kimataifa la Read International kuboresha jengo moja la
shule hiyo na kuliwekea samani kwa ajili ya matumizi ya maktaba.
“Read
International ni wadau wetu wakubwa hasa katika masuala ya elimu na
wamekuwa chachu ya kuleta maendeleo,kwa kutambua umuhimu wao tuliamua
kukaa chini na kuamua kukarabati jengo moja na kulifanya maktaba ili
vijana wetu wapate mahali pa kupatia maarifa zaidi”,alieleza.
Busunzu
alisema Acacia itaendelea kuunga mkono sekta ya elimu nchini kwa njia
ya kujenga miundombinu ya shule kama vile vyumba vya madarasa,nyumba za
walimu,vyoo na maabara na kutoa misaada kwa wanafunzi kupitia vifaa vya
elimu mfano vitabu,sare na ada kupitia programu ya CanEducate.
“Misaada
inayotolewa na Acacia katika sekta ya elimu ni sehemu ya sera ya
wajibikaji kwa jamii ya kampuni inayojikita katika kuhakikisha jamii
inakuwa endelevu kupitia sekta ya elimu na sera hiyo inachangia moja kwa
moja maono ya taifa hadi kufikia mwaka 2025 na malengo ya nchi ya
kuleta maendeleo endelevu kwa kuhakikisha jamii inapata elimu iliyo
bora”,alieleza.
Naye
Mwakilishi wa shirika la Read International linalojihusisha na masuala
ya elimu,Esther Kalwinzi mgodi wa Buzwagi ndiyo uliotoa shilingi milioni
22.4 kwa ajili kukarabati darasa kuwa maktaba.“Jumla
ya vitabu 1,278 vimehifadhiwa katika maktaba hii ambayo itahudumia
wanafunzi wapatao 290 na walimu 23 na jumla ya gharama za marekebisho ya
jengo hili,vitabu na samani za maktaba ni shilingi
22,442,953”,alifafanua Kalwinzi.
Kwa
upande wake,mgeni rasmi katika hafla hiyo,Mkurugenzi wa Mji wa
Kahama,Underson Msumba aliushukuru mgodi huo kwa kuendelea kuwa karibu
na jamii inayowazunguka na kushirikiana katika shughuli za maendeleo.
“Wakati
mwingine huwa nafikiria bila mgodi Kahama ingekuwaje,kwa kweli mgodi
umefanya juhudi nyingi katika kuboresha sekta ya elimu katika wilaya
yetu,ninaamini uwepo wa maktaba hii utawafanya wanafunzi kufanya vizuri
zaidi katika masomo yao”,alisema Msumba.
Aidha
aliwataka wanafunzi kuzingatia masomo yao huku akisisitiza kuwa elimu
ndiyo urithi pekee wa kudumu na wenye kubadilisha maisha yao.
Muonekano
wa jengo la maktaba katika shule ya sekondari Bugisha lililoboreshwa na
mgodi wa Buzwagi kwa kushirikiana na Read International - Picha zote na
Kadama Malunde - Malunde1 blog
Mkurugenzi
wa halmashauri ya wilaya ya Kahama Mji Underson Msumba,meneja mkuu wa
migodi ya Buzwagi na Bulyanhulu Benedict Busunzu ,viongozi mbalimbali wa
kata ya Mondo,walimu na wanafunzi wakiwa nje ya jengo hilo la maktaba
kabla ya kuzinduliwa rasmi
Mkurugenzi
wa halmashauri ya Mji wa Kahama,Underson Msumba akikata utepe kuzindua
rasmi jengo la maktaba katika shule ya sekondari Bugisha. Katikati ni
Meneja mkuu wa migodi ya Buzwagi na Bulyanhulu Benedict Busunzu.Wa
kwanza kushoto ni Mwakilishi wa shirika la Read International ,Esther
Kalwinzi akifuatiwa na diwani wa kata ya Mondo Kija Peja
Mwakilishi
wa shirika la Read International ,Esther Kalwinzi akionesha sehemu ya
kuangalia orodha/aina ya vitabu vilivyopo katika maktaba hiyo
Mkurugenzi wa halmashauri ya Mji wa Kahama,Underson Msumba akiangalia vitabu katika maktaba ya shule ya sekondari Bugisha
Mkurugenzi
wa halmashauri ya Mji wa Kahama,Underson Msumba na Meneja mkuu wa
migodi ya Buzwagi na Bulyanhulu Benedict Busunzu wakisoma vitabu ndani
ya maktaba ya shule ya sekondari Bugisha
Mkurugenzi wa halmashauri ya Mji wa Kahama,Underson Msumba akiangalia mandhari ya maktaba hiyo
Mkurugenzi
wa halmashauri ya wilaya ya Kahama Mji Underson Msumba,meneja mkuu wa
migodi ya Buzwagi na Bulyanhulu Benedict Busunzu ,viongozi mbalimbali wa
kata ya Mondo,walimu na wanafunzi wakiwa nje ya jengo la maktaba baada
ya uzinduzi
Mkurugenzi wa halmashauri ya wilaya ya Kahama Mji Underson Msumba akiwasisitiza wanafunzi kuzingatia masomo yao
Meneja
mkuu wa migodi ya Buzwagi na Bulyanhulu Benedict Busunzu akielezea
namna walivyoshirikiana na shirika la Read International katika
kufanikisha ukarabati wa jengo hilo la maktaba
Mwakilishi
wa shirika la Read International ,Esther Kalwinzi akizungumza wakati wa
hafla fupi ya uzinduzi wa jengo la maktaba katika shule ya sekondari
Bugisha
Mkurugenzi wa halmashauri ya wilaya ya Kahama Mji Underson Msumba
Mkuu
wa shule ya sekondari Bugisha Limbuzizi Magumba akiushuru mgodi wa
Buzwagi kwa kutoa shilingi milioni 22.4 kwa ajili ya ukarabati wa
maktaba katika shule yake
Wanafunzi wa shule ya sekondari Bugisha wakiimba shairi wakati wa hafla ya kuzindua maktaba katika shule hiyo
Mwanafunzi
Tedy Martine akisoma risala akisoma risala kwa mgeni rasmi.Alizitaja
miongoni mwa changamoto zilizopo katika shule hiyo kuwa ni upungu wa
viti na meza hali inayowafanya wakae wawili wawili lakini pia upungufu
wa walimu wa masomo ya sayansi.
Diwani
wa kata ya Mondo Kija Peja akiushukuru mgodi wa Buzwagi kwa kuendelea
kusaidia jamii na kuomba ushirikiano uendelee kuwepo.
Picha zote na Kadama Malunde - Malunde1 blog
Post a Comment