Mmoja
wa wakazi wa kijiji cha Ikengwa, Nade Laida, akibubujikwa machozi
wakati wa mkutano kati ya wanakijiji na msafara wa Waziri wa Maliasili
na Utalii Dkt. Hamisi Kigwangala kutokana na kile kilichoelezwa kuwa
mwanamke huyo ni mmoja wa waathirika wa mgogoro baina ya Pori la Akiba
Mkungunero na wananchi wa vijiji vinavyozunguka pori hilo.
Mmoja
wa wakazi wa kijiji cha Keikei Tangini ambaye jina lake halikufahamika
mara moja, akiwa ameshikilia bango linaloeleza kuwa mipaka ya Pori la
Akiba Mkungunero imesogezwa kwenye kijiji chao.
Naibu
Waziri wa Fedha na Mipango ambaye pia ni Mbunge wa Jimbo la Kondoa
Vijijini, Dkt. Ashatu Kijaji (katikati) akizungunza wakati wa mkutano
ulioitishwa na Waziri wa Maliaasili na Utalii Dkt. Hamisi Kigwangala
katika kijiji cha Keikei Tangini ili kusikiliza malalamiko ya wananchi
wa vijiji vinavyozunguka Pori la akiba Mkungunero kuhusu kumegwa kwa
maeneno yao na Pori hilo, wilayani Kondoa mkoani Dodoma.
Wakazi
waishio jirani na Pori la Akiba la Mkungunero lililoko Wilayani Kondoa
mkoani Dodoma, wameiomba Serikali iwarejeshee eneo la kilometa 12
kuanzia kwenye vijiji vyao kwenda ndani ya Pori hilo ambalo wanadai
limechukuliwa kinyemela na Wizara ya Maliasili na Utalii na kuathiri
maisha yao yanayotegemea kwa kiasi kikubwa kilimo na ufugaji.
Wakazi
wa vijiji vya Ikengwa, Keikei Tangini, Keikei na Kisondoko, wametoa
maombi hayo mbele ya Waziri wa Maliasili na Utalii Dkt. Hamisi
Kigwangala wakati alipofanyaziara katika vijiji hivyo vinavyozunguka
Pori hilo la Akiba ili kutatua mgogoro wa muda mrefu baina ya Pori hilo
na wananchi wanaolizunguka.
Wananchi
na viongozi wa vijiji hivyo wameeleza kuwa uwekaji wa mipaka ya Pori
hilo haukuwa shirikishi na kwamba maeneo makubwa ya vijiji yaliyokuwa
yakitumiwa na wananchi kwa shughuli zao za kilimo, ufugaji na makazi
yametwaliwa na kusababisha mgogoro huo.
Malalamiko
mengine ya wananchi hao ni kunyanyaswa na watumishi wa Pori la Akiba
Mkungunero kwa kupigwa, kunyang'anywa mifugo yao, na baadhi yao kudai
kuumizwa na baadhi ya wenzao kuuawa kwa risasi na askari wanaolinda Pori
hilo.
Kwa
Upande wake Naibu Waziri wa Fedha na Mipango, ambaye pia ni Mbunge wa
Jimbo la Kondoa Vijijini Dkt. Ashatu Kijaji, ameiomba Serikali kutumia
busara na kurejesha eneo lililochukuliwa kimakosa kutoka kwa wananchi
ili waweze kujiendeleza kiuchumi na kuishi kwa amani na utulivu.
"Najua
wewe ni mwadilifu ndio maana umeaminiwa na Mhe. Rais, najua utawatendea
haki wananchi wa vijiji hivi ili nao wajione ni wananchi halali katika
Taifa lao huru la Tanzania tukienda hatua kwa hatua bila kuvunja sheria
za nchi" alisisitiza Dkt. Kijaji
Amefafanua
kuwa maeneo yaliyochukuliwa na Pori hilo yalikuwa yakitumiwa na
wananchi kwa muda mrefu na kwamba mchakato wa kupandisha hadhi eneo hilo
kutoka Pori Tengefu hadi kuwa Pori la Akiba la Mkungunero
haukuwashirikisha wananchi.
Akijibu
Hoja za Wananchi hao, Waziri wa Maliasili na Utalii, Dkt. Hamis
Kigwangala, pamoja na kutoa elimu kuhusu umuhimu wa uhifadhi kwa ustawi
na maendeleo ya nchi, aliwahakikishia wananchi hao kwamba Serikali
itatafuta njia ya bora ya kuumaliza mgogoro huo kwa maslahi ya pande
zote mbili, wananchi na Serikali.
"Ni
lazima tutafute mahali ambapo tutabalance, maslahi ya umma na maslahi
mapana ya Taifa zima na niwahakikishie kuwa tutafanyakazi hiyo kwa
uadilifu, uzalendo mkubwa, lakini zaidi kwa kuzingatia maslahi yenu
wananchi wenzetu" Alisisitiza Dkt. Kigwangala.
Awali,
Meneja wa Pori hilo, Emmanuel Birasso, alieleza kuwa mchakato wa
kuanzisha Pori hilo la Akiba Mkungunero ulifuata taratibu za kisheria za
uanzishwaji wa mapori ikiwa ni pamoja na kuwashirikisha wananchi jambo
ambalo linapingwa na wananchi hao.
Alieleza
kuwa mpaka sasa takriban kilometa 118 za mpaka wote wa Pori umesimikwa
alama za mipaka na kuwaondoa watu wanaodaiwa kuvamia Pori hilo pamoja na
kuimarisha ulinzi na doria.
Pori
Tengefu la Mkungunero (Game Controlled Area) lilipandishwa hadhi na kuwa
Pori la Akiba la Mkungunero mnamo mwaka 1996 kwa Tangazo la Serikali
(GN) namba 307, likiwa na ukubwa wa kilometa za mraba 743.95.
Post a Comment