Share this PostPin ThisShare on TumblrShare on Google PlusEmail This


 BBC SWAHILI
Kampuni kubwa ya teknolojia Apple imethibitisha kwamba itanunua vipokea sauti na huduma ya kusikiliza muziki kupitia kwenye mtandao wa inteneti kutoka kampuni ya Beats Electronics katika makubaliano ya dola bilioni 3.

Hayo yakiwa ni makubaliano makubwa katika historia ya miaka 38 ya kampuni hiyo.

Hatua hiyo inaonekana kama jitihada ya kuiendeleza sifa ya Apple katika soko la kusikiliza muziki kwenye mtandao.

Pamoja na ununuzi huo, waanzilishi wa Beats Jimmy Lovine na msanii mtajika katika mtindo wa kufoka na Hip Hop Dkt. Dre watajiunga na kampuni hiyo ya kiteknolojia.

Je, Una Habari,Picha,Tangazo,Makala, Ushauri n.k.?Basi Wasiliana Nasi Simu/WhatsApp 0759 406 070

Post a Comment

 
Top