Share this PostPin ThisShare on TumblrShare on Google PlusEmail This
Mtoto aliyefanyiwa kitendo hicho jana lihifadhiwa  akisimulia namna alivyokuwa akifanyiwa ukatili huo
Shangazi wa mtoto huyo Upendo Ngongi akisimulia kwa machungu namna mtoto wa kaka yake alivyofanyiwa ukatili huo.
Kamanda wa Polisi mbeya Ahmed Msangi


Na EmanuelMadafa,Mbeya
Katika hali isiyokuwa ya kawaida Mtoto wa kiume wa  darasa la kwanza mwenye umri wa miaka saba, amekuwa akifanyiwa vitendo vya ukatili wa kijinsia kwa kuingiliwa kinyume cha maumbile(kurawitiwa) ndani ya kipindi cha mwaka mmoja.

Mtoto huyo ambaye jina lake limehifadhiwa, inadaiwa alianza kufanyiwa vitendo hivyo na mwanachuo Daudi  Anania umri unaokadiliwa kuwa 27 kutoka chuo cha Ufundi cha Veta kilichopo ndani ya Jiji la Mbeya, tangu akiwa na umri wa miaka sita kipindi hicho akiwa anasoma elimu ya awali.

Blog hii  lilifanikiwa kuzungumza na mtoto huyo, ambaye hivi sasa ameanza matibabu  baada ya vipimo kutoka kwa daktari wa hospitali ya Rufaa ya Mbeya kuonyesha ya kwamba mtoto huyo amethirika zaidi kwenye njia ya mkojo ambako kumekutwa na uvimbe na sehemu ya haja kubwa ikiwa tayari imeharibiwa.

Akisimulia mkasa huo, mtoto huyo amesema kuwa mwaka 2013 akiwa anaenda shule (elimu ya awali) njiani  alikutana na kijana huyo ambaye alimueleza ya kwamba waende wote nyumbani huku akimuhahidi kumnunulia biskuti na juice.

Amesema, wakiwa nyumbani kijana huyo alimpandisha kitandani na kumvua nguo kisha kumpaka mafuta kwenye sehemu ya haja kubwa na kisha kumuingili huku akimtaka asipige kelele na endepa atakahidi agizo hilo basi atammaliza kwa kisu ambacho inasemekana alikuwa amekiweka pembeni.

“Tulipofika nyumbani  tuliingia chumbani ,alinipandisha kitandani na kunivua nguo kisha kuniingilia huku akinitishia nisipige kelele kwani atanimaliza kwa kunichinja kwa kisu na alipomaliza alinifuta na kunipaka mafuta kisha kunirudisha nyumbani tena akinisisistizia ya kwamba nisiseme kwa mtu,”alisema mtoto huyo.

Aidha, kijana huyo aliendelea na mchezo huo mpaka siku ilipobainika baada ya majirani kuingiwa shaka na tabia ya mtoto huyo ambaye ilianza kubadilika kwa kuchelewa kurudi nyumbani  na mara alipowasili alikuwa akitembea kwa tabu tena macho yake yakiwa yameiva kwa kulia.

“Mara ya kwanza ya kubaini mtoto huyu amefanyiwa unyama huu ni Juni, 2013  tarehe sikumbuki siku hiyo alirudi nyumbani akiwa anatembea kwa tabu sana ndipo nilipomuita mama yake na kumweleza wasiwasi wangu ambapo tulimkalisha chini na alipobanwa alikiri kufanyiwa kitendo hicho na ndipo tulipomueleza shangazi yake,”alisema jirani ambaye hakuta jina lake liandikwe.

Shangazi wa mtoto huyo ambaye alijitambulisha kwa jina la Upendo Ngongi (31) mkazi wa eneo la Itiji Jijini Mbeya,aliambia blog hii  kwamba mara tubaada  ya kupata taarifa hiyo alifika kwenye eneo la tukio na kushuhudia mtoto huyo akiwa ameharibiwa.

“Nilipomkagua mtoto nilishuhudia unyama huo ulivyofanyika hivyo nilichukua jukumu la kumweleza baba wa mtoto ambaye ni kaka yangu ambaye alitutaka twende kituo cha polisi kutoa taarifa kisha tumpeleke mtoto hospitali,’’alisema.

Amesema, wakiwa njiani kuelekea kituo cha polisi alipigiwa simu na kaka yake ambaye ndiye baba wa mtoto na kumtaka warudi nyumbani na waachane na masuala ya polisi.

“Nilishtuka sana mara baada ya kusikia kauli ya kaka ikiniambia nirudi nyumbani niachane na masuala ya polisi, nilitii agizo lake na kurudi nyumbani lakini nilipomuhoji kwanini amechukua maamuzi haya aliniambia ya kwamba yeye hataki ugomvi na majirani,”alisema.

Amesema, kitendo cha kwenda polisi kitamletea yeye matatizo ya kugombana na majirani wakati wao si wenyeji wa Mbeya hivyo ni vema amuondoe mtoto kwa kumrudisha nyumbani Songea.
“kweli kaka alimrudisha mtoto nyumbani lakini mwezi wa kwanza (January 2014)alimrudisha Mbeya kwa ajili ya kuanza elimu ya darasa la kwanza huku tukiamini ya kwamba atakuwa amesahau tukio lile lililompata,”alisema.

Amesema, mtoto huyo alianza masomo yake na kuendelea vizuri mpaka juzi ambapo walishangaa kumuona mtoto huyo akirudi nyumbani akiwa analia tena akitembea kwa shida sana na ndipo walipombana na kumuuliza na kudai ya kwamba kijana yule aliyemfanyia ukatili mwaka jana amemfanyia tena.

“Kwa kweli tulishangaa kumuona mtoto akitembea tena kama kipindi cha awali na tulipombana kwa kumuhoji ndipo alipotueleza ya kwamba kijana Daudi amemuingilia tena na ndipo tulipochukua jukumu la kwenda kituo cha polisi”alisema.

Amesema, kwakua mtoto alikuwa amechafuliwa sana iliwabidi wamsafishe pasipo fikiria ya kwamba kitendo hicho kingepoteza ushahidi wenye nguvu.

Amesema, walifika kwenye kituo cha polisi na kuchukua PF3 ambayo ingemuwezesha mtoto huyo kutibiwa  na kwenda nayo hospitali ya Rufaa  ya Mbeya kitengo cha huduma ya haraka ambapo walimkuta daktari na kuwaeleza ya kwamba masaa 72 yalikuwa yameshapita tokea tukio lifanyike hivyo yeye binafsi hana msaada wowote ule.

“Mimi nilishangaa sana kusikia kauli hii kwani ni kweli masaa hayo yalikuwa yamepita lakini mbona hakumchunguza mtoto kwani kwa uwelewa wangu mdogo nikiangalia sehemu za siri za haja kubwa za mtoto naona njia iko wazi,”alihoji Shangazi huyo.

Ameongeza, kuwa  baada ya kuchoshwa na mizunguko isiyokuwa na matumaini iliwalazimu kurudi nyumbani bila ya mtoto kufanyiwa uchunguzi mpaka siku ya pili waliporudi, tena kwa msaada wa wanasheria na ndipo mtoto kufanyiwa uchunguzi na kubainika ya kwamba  njia ya haja kubwa ilikuwa imeharibiwa na sehemu ya haja ndogo ilikuwa na uvimbe.

Amesema, baada ya mtoto kupatiwa matibabu walirudi nyumbani na kuanza kuweka mitego ya kumbaini muhusika  na kufanikiwa kumkamata  na kumfikisha kwenye vyombo vya sheria polisi.
Afisa Mtendaji wa Kata ya Itiji, Leonard Magoma alikiri kupokea taarifa za tukio hilo na kwamba  serikali itasimamia suala hilo ili haki itendeke.

Hata hivyo Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Mbeya, Ahmed Msangi, alithibitisha kutokea kwa tukio hilo na kwamba mtuhumiwa amekamatwa, upelelezi unafanyika mara utakapokamilika mtuhumiwa atafikishwa mahakamani.
Mwisho.

Je, Una Habari,Picha,Tangazo,Makala, Ushauri n.k.?Basi Wasiliana Nasi Simu/WhatsApp 0759 406 070

Post a Comment

 
Top