| Kamanda wa Polisi Mbeya Ahmed Msangi |
Na Emanuel Madafa,Mbeya
Jeshi la polisi mkoa wa mbeya kwa kushirikiana na
askari wa nakonde nchini zambia linamshikilia jambazi mmoja aliyefahamika kwa
jina la jimmy nyilenda raia wa
zambia baada ya kujeruhiwa kwa kupigwa
risasi katika jaribio la unyang’anyi.
Tukio hilo limetokea mnamo tarehe 02.06.2014 majira ya saa 17:45
jioni katika eneo la mpakani kati ya tanzania na zambia [tunduma/nakonde].
Kamanda wa Polisi Mkoani Mbeya Ahmed Msangi amesema
kuwa watu wanaosadikiwa kuwa ni
majambazi walifyatua risasi ovyo kwa lengo la kuwapora pesa wabadilishaji fedha
wa eneo hilo na polisi wa tunduma [tanzania] na nakonde [zambia] walikabiliana
na majambazi hao.
Katika
majibizano hayo, majambazi watatu waliuawa wawili wakifahamika kuwa ni sikapwite boniphace
mfanyakazi wa council nakonde raia wa zambia na chapwa kipakwa raia na mkazi wa zambia na mwingine hakuweza kufahamika.
Aidha majambazi wengine waliweza kukimbia na jambazi
mmoja jimmy nyilenda raia wa zambia
amekamatwa akiwa mahututi baada ya kujeruhiwa kwa kupigwa risasi.
Katika tukio hilo silaha mbili aina ya ak-47 zenye namba 625562 na 1963ec58
zilikamatwa. Hata hivyo katika majibizano hayo raia wawili wa nakonde –zambia
walijeruhiwa na wamelazwa kituo cha afya tunduma.hakuna madhara kwa askari na
silaha zipo polisi nakonde zambia huku Juhudi za kuwatafuta majambazi waliokimbia
zinaendelea.
Kamanda wa polisi mkoa wa mbeya kamishina msaidizi
mwandamizi wa polisi ahmed z. Msangi
anatoa wito kwa yeyote mwenye taarifa za mahali walipo watuhumiwa hao wa tukio
la ujambazi azitoe katika mamlaka husika ili wakamatwe na hatua za kisheria
zichukuliwe dhidi yao.
Aidha anatoa wito kwa wafanyabiashara kuwa makini kwa
kuchukua tahadhari katika kazi zao.
MWISHO






Post a Comment