Share this PostPin ThisShare on TumblrShare on Google PlusEmail This
 Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akihutubia kwenye maadhimisho ya siku ya kupiga vita madawa ya kulevya yaliyoadhimishwa kitaifa leo Juni 26-2014 katika viwanja vya Ruanda Nzovwe Mkoani mbeya. 
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Mohammed Gharib Bilal. akipata maelezo juu ya athari za utumiaji wa madawa ya kulevya kutoka kwa Msanii Rehema Charamila (RC) wakati alipotembelea mabanda ya maonesho, kwenye maadhimisho ya siku ya kupiga vita madawa ya kulevya yaliyoadhimishwa kitaifa leo Juni 26-2014 katika viwanja vya Ruanda Nzovwe Mkoani mbeya. 

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Mohammed Gharib Bilal. Akionyeshwa baadhi madawa ya kulevya na Mkemia Daraja la kwanza Alois Ngonyani, alipotembelea mabanda ya maonesho kwenye maadhimisho ya siku ya kupiga vita madawa ya kulevya yaliyoadhimishwa kitaifa leo Juni 26-2014 katika viwanja vya Ruanda Nzovwe Mkoani mbeya.

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Mohammed Gharib Bilal akisalimiana na Msanii Rehema Charamila kwenye maadhimisho ya siku ya kupiga vita madawa ya kulevya yaliyoadhimishwa kitaifa leo Juni 26-2014 katika viwanja vya Ruanda Nzovwe Mkoani mbeya.

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Mohammed Gharib Bilal akisalimiana na Msanii Masanja Mkandamizaji kwenye maadhimisho ya siku ya kupiga vita madawa ya kulevya yaliyoadhimishwa kitaifa leo Juni 26-2014 katika viwanja vya Ruanda Nzovwe Mkoani mbeya. 
Baadhi ya wananchi wa Mkoa wa mbeya na baadhi ya Vijana walioathirika kutokana na kumia madawa ya kulevya wakiwa katika maandamano kwenye maadhimisho ya siku ya kupiga vita madawa ya kulevya yaliyoadhimishwa kitaifa leo Juni 26-2014 katika viwanja vya Ruanda Nzovwe Mkoani mbeya.
(Picha na OMR)

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akisalimiana na baadhi ya Wanafunzi wa shule mbalimbali za Mkoa wa Mbeya baada ya kuhutubia kwenye ya maadhimisho ya siku ya kupiga vita madawa ya kulevya yaliyoadhimishwa kitaifa leo Juni 26-2014 katika viwanja vya Ruanda Nzovwe Mkoani mbeya. 
Na EmanuelMadafa,Mbeya

MAKAMU wa Rais, Dk. Mohammed Gharib Bilal, amesema dawa za kulevya ni tishio,  kwa kuwa zinapunguza na kudhorotesha kasi ya maendeleo ya nchi.
Kadhalika, amesema wimbi la vijana wengi kukamatwa na kufunghwa nje ya nchi kutokana na kujihusisha na vitendo vya biashara haramu ya dawa za kulevya vinaleta taswira  mbaya na kulitia aibu taifa.

Aliyasema hayo jana Jijini hapa, wakati wa maadhimisho ya siku ya kupinga vita dawa za kulevya duniani, ambapo kitaifa yalifanyika mkoani Mbeya.
Akihutubia umati wa wananchi katika katika uwanja wa Ruanda Nzovwe Jijini hapa, Makamu wa Rais, Dk. Bilal alisema,dawa za kulevya ni tishio kwa maendeleo ya taifa kwa sababu hupunguza nguvu kazi ya taifa.

Amesema matumizi ya dawa za kulevya huzorotesha afya za watumiaji na huongeza  vitendo vya uhalifu  katika jamii, lakini pia husababisha gharama nyingine zisizo za lazima kwa taifa.
Alisema vitendo vya watanzania, hususani vijana kujihusisha na biashara ya kulevya ndani na nje ya nchi vimeendelea kwa kasi kubwa kutokana na taarifa za kukamastwa kwao.

“Takwimu za Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikano wa kimataifa, kuanzia mwaka 2006 hadi Aprili 2014 jumla ya watanzania 291  wanatumikia vifungo mbalimbali katika  nchi za China na Brazil baada ya kuhukumiwa vifungo kwa makosa ya  biashara  haramu za dawa za kulevya.” Alifafanua Dk. Bilal.

Aidha, ameongeza kuwa  katika kipindi cha mwaka 2011 hadi Mei 2014 kulikuwa na jumla ya watumiaji 1526 wa dawa za kulevya waliokuwa wakiendelea kupatiwa tiba kwa kutumia dawa Methadone katika hospitali ya Taifa Muhimbili, Mwananyamala na  Temeke.

Amesema kati ya watu hao waliobainika kutumia dawa hizo na kuanzishiwa matibabu, wanaume walikuwa 1321, huku wanawake idadi yao ikiwa ni 205.
Alisema athari nyingine zinazotokana  zinazxotokana na matumizi ya dawa za kulevya ni kuongezekas kwa maambukizi ya virus vya Ukimwi kutokana na waathirika kufanya ngono uzembe.

Dk. Bilal alisema kuwa, kutokanma na hali serikali imeendelea na jitihadfa za kupambana na tatizo hilo ambapo Januari 2009 hadi Mei 20014 jumla ya watuhumiwa 13,846 walikamatwa kwa kujihusisha na biashara hiyo haramu.

Amesema watu hao walikamtwa wakiwa na aina tofauti tofauti za dawa hizo ambazo ni Heroin kilo 966.06, Kokeini kilo 363.7,wakati dawa aina ya Mirungi kilo 45,734, huku bangi ikiwa ni tani 212.071.

Vile vile amesema, vikosi kazi vya kimataifa vya kupambana na uhalifu katika bahari ya Hindi vinavyopambana na dawa za kulevya na uharamia vijulikanavyo kama (Combained Task Force-150) vilifanikiwa kukamata jumla ya kilo 2300 za dawa za kulevya aina ya Heroin kuanzia januari hadi Mei 2014.

Dk. Bilali amesema  dawa hizo zilikusudiwa kuingizwa katika ukanda wa pwani wa Afrika Mashariki zikiswemo Tanzania, Kenya na Somalia.
Katika hali nyingine, Waziri wa nchi, ofisi ya Waziri Mkuu sera uratibu na Bunge, Wiliam Lukuvu, akimkaribisha mgeni rasmi katioka maadhimisho hahyo, alisema kati ya vijana zaidi ya 400 waliokamatwa katika nchi mbalimbali duniani wanahatari ya kuishia kunyongwa.

Katika maadhimisho hayo, Msanii maarufu wa muziki wa kizazi kipya, Rehema Chalamila, aliibua simanzi kubwa kwa wananchi waliohudhuria maadhimisho hayo baada ya kutoa ushuhuda wake wa namna alivyoweza kujiingiza kwenye utumiaji wa dawa hizo na madhara aliyoyapata kwake na familia yake.
Mwisho.

Je, Una Habari,Picha,Tangazo,Makala, Ushauri n.k.?Basi Wasiliana Nasi Simu/WhatsApp 0759 406 070

Post a Comment

 
Top