![]() |
| Baadhi ya wahamiaji haramu kutoaka Nchini Kongo na Burundi ambao wamekamatwa na maofisa wa uhamijia Mkoani Mbeya ambao wamekamtiwa Tunduma Wilayani Momba wakielekea Nchini Malawi. |
![]() |
| Mmoja wa wahamiji hao kutoka Mkoa wa Sidikifu Nchini Burundi Ndugu Chekabitu Byawombi akielezea namna walivyosafirishwa kutoka nchini mwao hadi hatua ya kukamatwa kwao Nchini Tanzania. |
Na EmanuelMadafa,Mbeya
DARA ya Uhamiaji Mkoani Mbeya imekili kuwa adhabu inayotolewa kwa watu wanaojihusisha na vitendo vya kuingiza wahamijai haramu nchini ni ndogo na haiwezi kukomesha vitendo hivyo .
Hatua inakuja kufuatia kuwepo kwa ongezeko la Idadi kubwa ya wahamiaji haramu wanaoingia Nchini Kupitia Mipaka ya Tanzania na Malawi pamoja na Zambia.
Akizungumza na Waandishi wa Habari Ofisi Kwake Afisa Uhamiaji Mkoa wa Mbeya Ndugu Asumso Achecha amesema sheria inayotumika sasa bado inatoa mianya ya baadhi ya watanzania kuendelea kujihusisha na biashara hiyo haramu.
Amesema sheria inayotumika kwa sasa ni ile ya mwaka 1995 ambayo imekuwa ikitoa adhabu ya faini ya shilingi laki Moja au jela mwaka mmoja kitendo ambacho hakizuii tatizo badala yake inaongeza tatizo kweni wengi wao wamekuwa wakilipa faini na kuachiwa huru.
Amesema kutokana na hali hiyo Idara ya Uhamiaji ipo katika mchakato wa kufanya maboresho hususani katika kipengele hicho cha sheria .
Hata hivyo amebainisha kuwa lengo la kutoa adhabu hiyo ni kuzuia au kupunguza kabisa tatizo hilo lakini mpaka mpaka sasa vitendo hivyo vimekuwa vikiendelea hasa kwa kuhusisha watanzania
Aidha Afisa Uhamiaji huyo amesema kuwa mpaka sasa jumla wahamiaji haramu 266 wamekamatwa mkoani mbeya kwa kosa la kuingia nchini bila wakiwemo watanzania watatu kwa kuanzia mwezi January hadi mwezi June.
Katika idadi hiyo nchi ya Ethiopia imetajwa kuwa na idadi kubwa ya wahamiaji waliokamatwa kutokana kuingia nchini bila kibali ambao ni 205 huku wakongo wakiwa 32 pamoja warundi 22.
Wengine wanne kutoka Somalia pamoja na Wamalawi wawili na Mkenya Mmoja ambao wote kwa ujumla wake walifikishwa mahakamani na kupewa adhabu mbalimbali ikiwemo vifungo.
Hata hivyo Afisa uhamiaji huyo amebainisha sababu za wahamiaji hao kuingia nchini bila husuani kwa mkoa huo ambao unatokana na mkoa wa mbeya kuunganisha Tanzania na nchi za kusini mwa afrika.
Amesema kutokana na hali hiyo watu hao wamekuwa wakitumia njia hiyo kupita kwenda Afrika kusini na baadaye kwenda nchi za Ulaya na wengine kubaki nchini hali ambayo imekuwa ikichangia kuongezeka kwa vitendo vya ugaidi pamoja na usambazaji wa madawa ya kulevya .
Kufuatia hali hiyo Asumso ametoa wito kwa wananchi mkoani kuhakikisha wanatoa taarifa za uwepo wa watu wasio wafaham pamoja na kuacha tabia ya kuwahifadhi watu haon kwa maslahi ya Taifa.
Asumso Achacha ameendelea kuwashukuru wananchi kwa ushirikano wanaoutoa kwa idara hiyo katika kuwabaini watu hao..
mwisho











Post a Comment