![]() |
| Meneja wa Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya (NHIF) Kanda ya Nyanda za Juu Kusini Dr. Mohamed Kiholile |
Na EmanuelMadafa,Mbeya
Jumla ya akina
mama wajawazito 67,542 wameandikishwa na kulipiwa jumla ya shilingi 699,156,000 kwa ajili ya
mchango wa mfuko wa afya ya jamii CHF kwa
Mkoa wa mbeya.
Uandikishaji huo ni sehemu ya mradi KFW
ambao unalengo la kupunguza vifo vya akina mama kama ilivyo katika mpango wa
maendeleo wa millenia namba 5 ili kufikia malengo mwaka 2015.
Meneja wa Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya Nhif Kanda ya Nyanda za Juu Kusini Daktari Mohamed
Kiholile amesema utekelezaji wa Chf kwa mkoa wa mbeya umepata nguvu kubwa kutokana na kuwepo kwa mradi wa KFW .
Amesema mradi huo
unaendeshwa na mfuko wa taifa wa bima ya afya
ukishirikiana na Benki ya
maendeleo ya watu wa ujerumani ambapo lengo ni kuboresha afya
ya akinamama wajawazito na watoto sanjali na kuimarisha afya kwa ujumla.
Amefafanua kuwa zaidi ya shilingi milioni 650
zimekwisha lipwa kwenye
Halmashauri fedha ambazo nii muhimu sana katika kuboresha huduma za afya maeneo ya vijijini na mijini.
Hata hivyo Meneja huyo ameelezea changamoto zilizopo
katika mradi wa Kfw ni pamoja na mapungufu ya utunzaji
takwimu za kinamama wa Kfw
walioandikishwa hasa kwenye ngazi za
vito kama zahanati na vituo vya afya.
Changamoto nyingine ni suala la ugawaji wa kadi za
CHF kwa kinamama wa mradi Kfw
waliokoma uanachama wa NHIF kuwa umekuwa wa kusuasua na hauendani na kasi ya uandikishaji .
Mwisho.








Post a Comment