![]() |
| Bi.Mariam Ibrahim akiwa na mumewe |
Na EmanuelMadafa
Afisa mmoja mwandamizi katika wizara ya maswala ya kigeni
nchini Sudan amesema kuwa mwanamke aliyepewa hukumu ya kifo kwa kubadili dini
yake ya kiislamu,Meriam Ibrahim atawachiliwa huru katika kipindi cha siku
chache zijazo.
Abdullahi Alzareg ambaye ni katibu katika wizara hiyo amesema kuwa Sudan
inatilia maanani uhuru wa kuabudu na kwamba serikali itamtetea mwananmke huyo.
Kumekuwa na shutma za kimataifa kuhusu hukumu aliyopewa mwanamke huyo.
Meriam Ibrahim anazuiliwa katika jela moja ambapo alijifungua mtoto wa kike
juma hili.
Ameolewa na mkristo na pia amehukumiwa kuchapwa viboko mia moja kwa kuzini
kwa sababu mwanamke wa kiislamu kuolewa na mkristo ni haramu kulingana na
sheria za Sudan.CHANZO BBC SWAHILI







Post a Comment