Share this PostPin ThisShare on TumblrShare on Google PlusEmail This
Mkuu wa Mkoa wa Mbeya Ndugu Abbas Kandoro  akitoa shukrani kwa Askofu Mkuu wa Kanisa hilo pamoja na Kamati ya  inayosimamia ugawaji vyandurua hivyo chini ya Mkurugenzi wa Kituo cha Utafiti Mbeya(MMRC) Dr.Leonard Maboko 
Askofu Mkuu  wa Kanisa la Tanzania Assemblies of God ( TAG) Dr.Barnabas Mtokambali  mwenye suti Nyeusi akimkabidhi Vyandarua Mkuu wa Mkoa wa Mbeya Ndugu Abbas Kandoro  Makabidhiano yaliyofanyika katika ukumbi wa mikutano wa Hospital ya Rufaa Mbeya na kuhudhuria na baadhi ya wachungaji wa kanisa hilo pamoja na uongozi wa Hospital na watumishi baadhi



Askofu Mkuu  akionyesha baadhii ya vyandurua hivyo mbele wa washiriki katika hafla hiyo
Mkuu wa Mkoa wa Mbeya pamoja na Askofu Mkuu wa Kanisa hilo na Uongozi wa Hospital ya Rufaa ya Mbeya wakishiriki Maombi ya pamoja katika kuuombea mkoa wa mbeya pamoja na shughuli nzima ya kuelekea katika kilele cha sherehe hizo za Tag
Mwenyekiti wa Kamati ya Maandali ya shughuli za ugawaji wa Vyandarua hivyo ambaye pia ni Mkurugenzi wa Kituo cha Utafiti cha( MMRC) Dr.Leonard Maboko  akizungumza katika hafla hiyo.

Na EmanuelMadafa,Mbeya
KANISA la Tanzania Assemblies of God(TAG),  limetoa jumla ya vyandarua 8550 vikiwa na thamani ya shilingi milioni 280 katika hospitali na vituo vya afya 117  kwa mikoa mitatu ya Nyanda za juu kusini.

Sanjali na utoaji huo wa vyandarua pia kanisa hilo linatalajia kutoa damu katika benki ya damu salama Mkoani Mbeya ambapo zaidi ya wachungaji 800  wa kanisa hilo watahusika katika shughuli hiyo.

Akikabidhi  msaada huo leo   kwa Mkuu wa Mkoa wa Mbeya Abassi, Askafu Mkuu wa Kanisa hilo Dr. Barnabas Mtokambali, amesema utoaji msaada huo unaenda sambamba na maadhimisho ya miaka 75 ya uanzishwaji wa kanisa hilo nchini Tanzania mwaka 1939.

Amesema, TAG ni sehemu ya jamii kwani linatambua ukubwa wa tatizo la ugonjwa wa maralia  hivyo ni vema likaunga mkono juhudi za serikali katika kufikia malengo ya milenia kwenye mapambano dhidi ya ugonjwa huo.

Amesema, ugonjwa wa maralia umekuwa ukiligharimu Taifa kwa kupoteza watoto chini ya miaka mitano  na mama wajawazito hivyo pamoja na kanisa kutoa huduma ya kiroho  imeona ni vema ikachangia sehemu iliyotolewa na waumini wa dhehebu hilo katika kuokoa kizazi hicho.
Amesema wanatambua kuwa suala la utoaji huo wa vyandurua hauwezi kupunguza kabisa tatizo lakini kwa kiasi hicho kutasidia kuokoa kwa kiwango kikubwa changamoto ya uhaba wa vyandarua. 
Amesema,  vyandarua 1300 vitapelekwa Mkoani Rukwa kwa ajili ya Hospitali 3 na vituo vya afya na Zahanati zinazolaza wagonjwa  22  huku  vyandarua 3100 vitasambazwa Mkoani Njombe kwa ajili ya Hospitali 11 na vituo vya afya 25.

Amesema, vyandarua 4150 vitabaki Mkoani Mbeya kwa ajili ya Hospitali 20 na vituo vya afya na Zahanati  36.

Amesema, vyandarua vitakavyogawiwa  Mkoani Mbeya vimo  vyandarua 650 vya hospitali ya Rufaa ya Mbeya ambapo kati yake 500  ni kwa ajili ya hospitali kuu na 150 ni kwa ajili ya hospitali ya wazazi ya Meta.

Aidha, amesema kuwa idadi ya vyandarua vinavyogawiwa katika kila hospitali na Vituo vya afya kwa mikoa yote mitatu imefanyiwa upembuzi wa idadi ya vitanda vilivyomo ndani ya hospitali hizo na kwenye vituo vya afya.

Akipokea  vyandarua hivyo  Mkuu wa Mkoa wa Mbeya, Abbasi Kandoro amesema kitendo kilichofanywa na kanisa hilo kimeidharirishia jamii ya kwamba fedha zinazotolewa na waumini kama sadaka zinatekeleza agizo la mungu la kuyasaidia makundi muhimu.

Hata hivyo Mkuu huyowa Mkoa wa Mbeya ametumia fursa hiyo kulitaka kanisa hilo kuendelea kutoa wito wa waumini na jamii kwa ujumla kuhakikisha wanaachana na tabia ya kutumia madawa ya kulevya  aina ya banki pamoja na pombe haramu.

 mwisho

Je, Una Habari,Picha,Tangazo,Makala, Ushauri n.k.?Basi Wasiliana Nasi Simu/WhatsApp 0759 406 070

Post a Comment

 
Top