Share this PostPin ThisShare on TumblrShare on Google PlusEmail This
Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi CCM Mkoa wa Mbeya ambaye pia ni Naibu Waziri wa Kilimo Ushirika na Chakula (Mb) akizungumza na Jumuiya  ya Uvccm Mkoa wa Mbeya pamoja na viongoizi wa jumiya hizo toka mikoa mbalimbali Nchini ambao wamekutana jijini Mbeya kwa mualiko wa kuhudhuria sherehe za kuwasimika  Makamanda wa Mkoa huo sherehe ambazo zitafanyika  Julai 6 mwaka huu katika viwanja vya CCM Ruanda Nzovwe jijini hapa(.PICHA NA KENETH NGELESI)
Mwenyekiti Uvccm Mbeya Amani Kajuna akizungumza katika Mkutanao huo wa Baraza .
Wajumbe wakiwa makini kusikiliza yanayojili katika Mkutano huo
Katibu wa Hamasa Chipukizi Taifa ambaye pia ni Mjumbe wa Bunge Maalumu la Katiba Ndugu Paul Makonda akitoa neno la nasaha kwa wajumbe waliohudhuria mkutano huo toka Mbeya na Mikoa Mbalimbali Nchini.
Katibu wa Mwenezi Mkoa wa Mbeya ambaye pia ni Diwani Kata ya Bagamoyo Wilayani Rungwe Ndugu Bashiru Madodi  akizungumza na vijana wa jumuiya hiyo.
Mjumbe wa Mkutano Mkuu Taifa Uvccm Ndugu Nwaka Mwakisu 
Msanii wa Bongo Movie Steven Nyerere ambaye nae ni miongoni mwa wageni walioalikiwa katika Mkutano huo pamoja na sherehe za usimikaji Makamnda 11 wa Mbeya .
Mjumbe wa Baraza kuu Uvccm toka Mkoani Tanga  Husna Sekiboko akitoa neno fupi kwa wajumbe wa mkutano huo.
Serebuka Time
Na EmanuelMadafa,MBEYA

Jumuiya ya Umoja  wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi, UVCCM, umetakiwa kuacha tabia ya kukubali kutumika na baadhi ya wanasiasa wenye uchu wa kuwania madaraka ya urais.

Imeelezwa kuwa endapo umoja huo utakubali ushawishi kutoka kwa wanasiasa hao   iko hatari kubwa ya jumuiya hiyo kusambaratika .

Tahadhari hiyo imetolewa na Makada mbalimbaliwa CCM na UVCCM kwenye Mkutano wa Baraza Kuu la umoja huo Mkoa wa Mbeya uliofanyika kwa siku moja mjini hapa na kuhudhuriwa na Wenyeviti na Makatibu wa UVCCM kutoka mikoa yote ya Tanzania Bara na Zanzibar.
Akizungumza katika Mkutano huo wa baraza Katibu Mwenyezi wa CCM mkoa wa Mbeya, Ndugu  Bashiru Madodi, amesema endapo tabia hiyo itaendelea kuna hatari kwa UVCCM kusambaratika hata kabla ya uchaguzi mkuu ujao hii ni kutokana na kuongezeka kwa makundi ndani ya umoja huo.

Hata hivyo Mwezi huyo amebainisha kuwa kama watakubali hali kunauwezekano mkubwa wa jumuiya hiyo kuto fika hata Mwezi wa Nne mwakani kama wataendelea kukumbatioa tabia hiyo .

Amesema ipo dalili kubwa ya baadhi ya wajumbe wa baraza hilo kuonyesha waziwazi juu ya kuonyesha wazi kujikita katika kundi Fulani la watu wanao taka kuingia Ikulu.

Amesema watu hao wanaotangaza nia wanawafuata kwa sababu wanajua kuwa bila ya kuwashirikisha vijana hao kamwe hawezi kufanikisha malengo yao kwa sababu ya vijana kuwa na  nguvu ndani ya chama  hivyo amewataka kuwa  makini kwa kutumia nguvu na ushawishi wao  vizuri.

Naye  Katibu wa Hamasa wa UVCCM Taifa, Paul Makonda, amesema tatizo kubwa linaloukabili uomoja huo kwa sasa ni uwepo wa wanachama wasiojitambua kisiasa ambao wamekubali kuwekwa mifukoni na wanaotaka kuingia Ikulu hali inayosababisha kukosa ujasiri katika matendo na kauli zao na hivyo kila wanalolifanya lazima waseme wametumwa na fulani.

Mwenyekiti wa UVCCM Mkoani Mbeya, Amani Kajuna, amesema vijana wanapaswa kusubiri maamuzi ya chama kuhusu mgombea atakayeipeperusha bendera ya CCM kwenye uchaguzi ujao na kuunga mkono uamuzi huo badala ya kujiingiza kwenye makundi yanayohatarisha uhai wa umoja huo. 

Amesema umoja mshikamano ndio utakawezesha chama kupata kiongozi bora anayehitajika pamoja na kuendelea kukipa nguvu chama.

Mjumbe wa NEC Zanzibar, Nadya Juma Mohammed, amewataka vijana kutambua kuwa harakati za uchaguzi zinazohatarisha uhai wa UVCCM ni tukio la kipindi kifupi hivyo wanapaswa kuwa makini na wasikubali kugawanywa na wanasiasa hao kwa sababu uhai wa umoja huo unahitaji nguvu yao ya pamoja kwa muda mrefu.

Wakizungumzia sakata la Ukawa,Katibu wa CCM Wilaya ya Ileje, Luciano Mbossa , aliwataka vijana  wa CCM kupambana na kundi la Ukawa kwani ndio saizi yao na kuwaachia wazee wa CCM kutangaza ilani ya chama na utekelezaji wa sera kwa wananchi.


Hata hivyo,  akifungua mkutano huo, Mwenyekiti wa CCM mkoani Mbeya, Godfrey Zambi, aliwataka UVCCM kutokubali kununuliwa na wanasiasa katika kipindi hiki cha kuelekea uchaguzi mkuu ili kuepusha kupitisha wanasiasa wasiokuwa na uwezo.

Mwisho


Je, Una Habari,Picha,Tangazo,Makala, Ushauri n.k.?Basi Wasiliana Nasi Simu/WhatsApp 0759 406 070

Post a Comment

 
Top