![]() |
| Mganga Mkuu wa Mkoa wa Mbeya Daktari Sefu Mhina |
![]() |
| Baadhi ya wakuu wa Wilaya |
Na EmanuelMadafa,Mbeya
Viongozi Wakuu wa Mkoa na Wilaya Mkoani Mbeya wamekutana jijini Mbeya na kuweka maadhimo kadhaa yatakayo uwezesha Mfuko wa Afya jamii CHF kufikia malengo yake ya asilimia 30 ya wananchi kujiunga na mfuko huo mara ifikapo mwezi Desemba Mwaka huu.
Wadau hao ni pamoja na Wakuu wote wa Wilaya Mkoani Mbeya
, Wakurugenzi wa Halmashauri na sanjali na viongozi wa Mkoa wa Mbeya pamoja na
waganga wakuu .
Akitoa maadhimio ya Mkutano huo Meneja wa Mfuko wa Taifa
wa Bima ya Afya (NHIF) Kanda ya Nyanda za Juu Kusini Daktari Mohamed Kiholile
amesema kuwa katika mkutano wakuu hao wameweka maadhimio 17 ambayo yatatakiwa kutekelezwa na Mfuko huo wa Taifa NHIF kwa kushirikiana na viongozi hao .
Amesema moja ya Maadhimio hayo ni pamoja na kuhakikisha kuwa halmashauri zote za mkoa huo
zinaimarisha upatikanaji wa dawa na
vifaa tiba sanjali na kuongeza usajili wa wanachama kwa kuwahusisha waratibu kata elimu na wakuu wote wa shule.
Amesema adhimio jingine ni kuhakikisha kuwa kila halmashauri inajiwekea
mikakati ya kuwapiga picha wanachama
wapya wa CHF kwa lengo la kupunguza gharama
hali ambayo itachangia kwa wao kuwahamasika kujiunga na Mfuko huo.
Hata hivyo Meneja
huyo wa Bima ya Afya amesema kuwa wadau hao pia wameutaka mfuko wa Taifa wa
Bima ya Afya NHIF kuhakikisha
inafanya mchakato wa haraka wa
ubadirishaji wa sheria ya CHF sanjali na utoa wa taarifa kwa wadau hao juu ya
wapi wamefikia katika mchakato huo.
Pia amesema kuwa mkakati mwingine uliwekwa na wadau hao ni kuhakikisha kuwa kila wanapokutana wanapeana mrejesho wa maadhimio yaliyopita
sanjali na utekelezaji wake.
mwisho











Post a Comment