Share this PostPin ThisShare on TumblrShare on Google PlusEmail This
Askofu Mkuu wa Kanisa la TAG, Dr. Barnabas Mtokambali,akizungumza na waandishi wa Habari jijini Mbeya kuhusiana na sherehe za miaka 75 ya kuanzishwa kwa kanisa hilo zitakazofanyika Mkoani hapa na kuambatana na shughuli mbalimbali likiwemo suala la uchangiaji damu.
Baadhi ya wachungaji wa wa kanisa hilo wakiwa makini kumsikiliza Askofu Mkuu wa Kanisa hilo. 
Na EmanuelMadafa,Mbeya

Askofu Mkuu wa Kanisa la Tanzania Assemblies Of God  (TAG) anatalajiwa kuongoza wachungaji  wapatao 8000 kutoka Maeneo Mbalimbali Nchini kwa ajili ya shughuli ya uchangiaji Damu Katika kituo cha   damu salama  Kanda ya Nyanda za Juu kusini Mbeya.

Akizungumzia hilo, Askofu Mkuu wa Kanisa la TAG, Dr. Barnabas Mtokambali, amesema wachungaji hao wakiongozwa nayeye mwenyewe watachangia damu hiyo kwa hiari lengo kuu likiwa ni kuokoa uhai wa watu ambao hupoteza maisha kutokana na  kupungukiwa damu.

Amebainisha kuwa  kundi la kinamama wajawazito,watoto na majeruhi wa ajali wamekuwa wanahitaji damu nyingi mara wanapopata matatizo ya maradhi na ajali hivyo ni vema wao wakajitolea ili kupunguza  idadi ya vifo hivyo.

Aidha, Askofu Mtokambali, amesema zoezi hilo litaanza na wachungaji 800 ambapo kama mungu atakuwa amesaidia wahusika wote wakakidhi vigezo na masharti basi benki ya damu itakuwa imepokea lita 400.

Amesema, wachungaji wengine 4500 kutoka maeneo mbalimbali ya ndani na nje ya nchi wataungana na wenzao kwenye zoezi hilo mara watakapokuwa wamewasili.

Amesema, tayari kanisa limefanya taratibu zote za mawasiliano na ofisi ya Kanda kitengo cha Damu Salama kilichopo Hospitali ya Rufaa ya Mbeya na kwamba zimekamilika.

Hata hivyo, amewaomba wahusika wa kitengo hicho kujipanga vizuri kwani matumaini yake ni kwamba mbali na wachungaji hao wapo baadhi ya watu ambao nao watahitaji kuunga mkono zoezi hilo hivyo ni vema wakajipanga vizuri kwa vifaa pamoja na watoa huduma.


Mwisho.

Je, Una Habari,Picha,Tangazo,Makala, Ushauri n.k.?Basi Wasiliana Nasi Simu/WhatsApp 0759 406 070

Post a Comment

 
Top