Share this PostPin ThisShare on TumblrShare on Google PlusEmail This
Ripoti kutoka kaskazini-mashariki mwa Nigeria zinaarifu kuwa kundi la wapiganaji Waislamu la Boko Haram, limefanya mashambulio mawili makubwa katika siku chache za karibuni ambapo watu karibu 100 wameuwawa.
Kiongozi mmoja katika jimbo la Borno alisema kuwa wapiganaji waliuwa wauza samaki karibu 50 karibu na kijiji cha Doron Baga, kando ya Ziwa Chad.
Alisema wapiganaji wa Boko Haram wameweka kizuizi kwenye njia ya kuelekea Chad na kuwakamata wachuuzi waliokuwa wakienda kununua samaki.
Katika tukio jengine hapo awali watu karibu 50 waliripotiwa kuwa waliuwawa karibu na mpaka wa Cameroon pale Boko Haram walipovamia kijiji cha Azara Kuya, siku ambapo soko huwa na watu wengi.


Je, Una Habari,Picha,Tangazo,Makala, Ushauri n.k.?Basi Wasiliana Nasi Simu/WhatsApp 0759 406 070

Post a Comment

 
Top