Share this PostPin ThisShare on TumblrShare on Google PlusEmail This
Mkuu wa Wilaya ya Mbeya Profesa Norman Sigalla akizungumza na wajasilimali wa Mkoa wa Mbeya katika semina iliyoandaliwa na Benki ya Posta  (TPB)Tanzania katika ukumbi wa Mikutano Mtenda.


Wajasilimali wakiwa makini kumsikiliza mgeni rasmi




Na Emanuel Madafa,Mbeya
SERIKALI Mkoani Mbeya imezitaka Taasisi za kifedha (Mabenki) kuhakikisha wanaanzisha kitengo maalumu cha  kuwawezesha wafanyabiashara kutambua aina gani ya miradi wanatakiwa kuanzisha  ili kuwalahisishia kupata mikopo  katika taasisi hizo.
Kauli hiyo imetolewa leo jijini Mbeya na Kaimu Mkuu wa Mkoa wa Mbeya Profesa Norman Sigalla wakati akizindua mafunzo kwa wajasilimali yaliyoandaliwa na Benki ya Posta Tanzania yaliyofanyika katika ukumbi wa Mtenda ambapo wafanyabiashara waliopota fursa ya kuhudhuria semina hiyo ni zaidi ya 150.
Amesema kumekuwepo na changamoto kubwa kwa wafanyabiashara juu uanzishwaji miradi ya biashara hivyo umefika wakati kwa taasisi hizo kuanzisha dawati maalumu litakalo husika moja kwamoja na kusaidia wafanyabiashara hao katika eneo la maandiko ya miradi.
Amesema kuwepo kwa kitengo hicho pia  kutasaidia kuepusha wateja wao kurubuniwa na watu wan je ambao wamekuwa wakiwashauri tofauti na malengo ya mkopo.

Amesema  baadhi ya wafanyabiashara wamekuwa wakikwama katika kutimiza malengo yao ya kibiashara kutokana na udanganyifu wa maandiko ya shughuli anayokusudia kuifanya hivyo suala hilo litaondoa migongano hiyo.

Aidha amesema,ni vema andiko mradi likaenda sambamba na uhalisia wa shughuli ya kibiashara inayokusudiwa kufanywana mlengwa, ambayo pia itakuwa imekidhi viwango vya ubora utakaoendana na ushindani wa soko la ndani na nje ya nchi

Naye Mkurugenzi mtendaji wa Benki ya Posta, Sabasaba Mushingi, alisema lengo la benki hiyo kutoa mafunzo kwa wafanyabiashara na wajasiriamali zaidi ya 150 katika Mkoa wa Mbeya ni kuwawezesha kujua umuhimu wa huduma za kibenki hususani mikopo.

Amesema Benki hiyo ya posta imejitahidi kwa kiwngo kikubwa katika  kupunguza suala la ukubwa wa viwango vya riba vinavyotolewa na mabenki nchini,ambapo kwa  benki ya hiyo  ndiyo imeweza  kuwa na riba ndogo kuliko mabenki mengine kwa hapa nchini.
Mwisho.
Mkurugenzi mtendaji wa Benki ya Posta, Sabasaba Mushingi, 



Mgeni rasmi katika picha ya pamoja n wafanyakazi wa benki ya posta Tanzania Mkoa wa Mbeya

Je, Una Habari,Picha,Tangazo,Makala, Ushauri n.k.?Basi Wasiliana Nasi Simu/WhatsApp 0759 406 070

Post a Comment

 
Top