![]() |
| Mkuu wa shule hiyo ya Mbozi yenye kidato cha kwanza hadi sita, Eliya Msyaliha, akionyesha baadhi ya vifaa vilivyo tolea na wafadhiri hao. |
![]() |
| Mwalimu wa masomo ya Sayansi katika shule hiyo Sijali Mpesya akiwa na wanafunzi wake |
Na Mwandishi wetu,Mbozi.
Umoja wa Wakristo wa kanisa la Muhlaker lililopo katika mji wa
Wurttemburg, nchini Ujeruman limetoa msaada wa vifaa mbalimbali vya
masomo ya sayansi kwa shule ya sekondari ya Mbozi, vyenye thamani ya mamilioni
ya fedha.
Kadhalika, shule hiyo, mbali na kupewa vitabu vya masomo yote
yaliyo kwenye mkondo wa sayansi, pamoja na vifaa mbalimbali vya kisasa vya
maabara, pia imepokea msaada wa fedha kiasi cha sh.mil 11.
Akizungumza na waandishi wa habari ofisini kwake jana, Mkuu wa
shule hiyo ya Mbozi yenye kidato cha kwanza hadi sita, Eliya
Msyaliha, alisema vifaa hivyo vimetolewa kwa nyakati
tofauti kupitia program ya ushirikiano kati ya wafadhili hao na shule.
Amesema shule hiyo inayomilikiwa na kanisa la Moravian Tanzania
kusini M agharibi kwa muda mrefu limekuwa na utaratibu wa kushirikiana na
wakristo hao wa nchini Ujerumani.
Ameongeza kuwa mbali na vifaa, lakini pia kumekuwa na program
mahususi ya wakristo wan chi hiyo na washirika wao kutoa msaada wa walimu wa
masomo ya sayansi, ambao mara kadhaa huja kufanya kazi shuleni hapo.
Aidha, amesema kuwa wafadhili wengine wa Mission 21 wa nchini
Ujerumani nao kwa upande wao wamesaidia miundombinu ya majengo kwa kujenga
nyumba za walimu za muundo wa nyumba moja ndani ya tatu.
Amesema kutokana utajiri huo wa msaada wa vifaa hivyo vya masomo
ya sayansi, shule hiyo imeamua kusaidia wanafunzi wa shule za jirani kuja
kujifunza kwa vitendo hasa wakati huu wa likizo.
Amesema hali hiyo imeipunguzia shule hiyo mzigo hivyo kutumia
fursa hiyo kujikita zaidi kusaidia waqnafunzi kuongeza uelewa, ambapo sasa
wanafunzi wote wale wa bweni na kutwa hupata chakula shuleni hapo.
Mwisho.



















Post a Comment