Share this PostPin ThisShare on TumblrShare on Google PlusEmail This
Mwigizaji wa filamu Ummy Wenslaus ‘Dokii’ amefunguka kuwa ndani ya mwaka 2014 hajapata mwanaume wa kuendana naye hivyo endapo akibahatika kupata mwenye upendo wa dhati mwaka huu, atampa kila kitu anachokihitaji.
Akipiga stori na paparazi wa GPL, Dokii alisema kitu kikubwa kilichomfanya awatoe wanaume moyoni kwa mwaka 2014 ni kutokana na wengi wao kutokuwa na upendo wa dhati.
“Siwezi kuwa na mpenzi wakati kila siku naona wenzangu wanalia, sijui nitapata wapi mwanaume mwenye upendo, wengi wapo kwa ajili ya kufanya ngono na mwisho wa siku wanakuumiza,” alisema Dokii.

Je, Una Habari,Picha,Tangazo,Makala, Ushauri n.k.?Basi Wasiliana Nasi Simu/WhatsApp 0759 406 070

Post a Comment

 
Top