Share this PostPin ThisShare on TumblrShare on Google PlusEmail This

Madalali wa mahakama  Kampuni ya Jagro enterprises limited wakiendelea na shughuli za ufungaji wa kitio hicho  cha Mek One kilichopo Tukuyu Mbeya.




Na Emanuel Madafa,Mbeya.



MAHAKAMA Kuu leo, imekifunga kituo cha mafuta ya Petrol na Dizeli cha Mek One kilichopo Wilayani Rungwe, baada ya kukiuka amri ya mahakama hiyo iliyokitaka kituo hicho kusitisha huduma mpaka kesi ya msingi namba ­­6/2013 iliyopo katika mahakama ya Wilaya ya Rungwe itakapotolewa maamuzi.



Akizungumza na waandishi wa habari ofisini kwake, Msajili wa mahakama Aron Lyamuya, amesema, kituo hicho ambacho kinamilikiwa na Halmashauri ya Wilaya ya Rungwe, kiliingia mgogoro na Kampuni ya mafuta ya  GAPCO na  kuvunja mkataba hali iliyomfanya mmiliki huyo kufungua kesi katika mahakama ya Wilaya ya Rungwe



Amesema, wakati kesi hiyo inaendelea halmashauri  hiyo imeingia mkataba mpya na Kampuni ya mafuta ya Mek One, jambo lililomsukuma mmiliki wa awali ambaye ni GAPCO kufikisha barua  ya malalamiko kwenye  mahakama kuu.



Amesema, Oktoba 8, 2013, mahakama kupitia hukumu iliyotolewa na Jaji Atuganile Ngwala, iliitaka halmashauri ya Rungwe, kutofanya  jambo lolote katika kituo hicho, lakini inaonekana amekaidi amri hiyo hivyo, mahakama imempa dahama Kampuni  ya JAGRO kukifunga kituo hicho.



Aidha, amesema kuwa sambamba na kukifunga kituo hicho pia, mahakama hiyo inatarajia kuwafungulia kesi, mkurugenzi wa halmashauri ya Rungwe Veronica Kessy na mkurugenzi wa Kampuni ya Mek One Mohamed Awadhi kwa kosa la kukiuka amri ya mahakama.



Hata hivyo, akikifunga kituo hicho cha mafuta, Mkurugenzi wa Kampuni ya Jagro inayoshughulika na masuala ya udalali Mkoa wa Mbeya,Maulid Hamis ,amesema wao wanatekeleza agizo la mahakama, ambalo limewapa dhamana ya kukifunga kituo hicho, pia ni moja ya majukumu yanayofanywa na kampuni hiyo.



Mwisho.




JAMIIMOJABLOG

Je, Una Habari,Picha,Tangazo,Makala, Ushauri n.k.?Basi Wasiliana Nasi Simu/WhatsApp 0759 406 070

Post a Comment

 
Top