Share this PostPin ThisShare on TumblrShare on Google PlusEmail This


Peter Nzito


Stori: Saimeni Mgalula,Mbeya
 Kijana mmoja Stivini Nzito (28) Mkazi wa mji wa Uyole,Kata ya Igawilao Wilayani Mbeya Mjini Mkoani hapa,amesimulia jinsi maajabu yalivyotaka kumtokea baada ya kupotea kwa mdogo wake Peter Nzito katika mazingira ya kutatanisha.

Akizungumza na Paparazi wetu hivi karibuni Nyumbani kwake,kijana huyo alisema hofu kubwa ni kabla ya kupotea kwa mdogo wangu,alipotea jirani yangu ambaye hakumtaja kwa jina iia alikuwa ni mfanya biashara wa kuuza nguo kwa kutembeza .

‘’Ambaye naye alipotea kama mdogo wangu na akaja kupatikana Tunduma akiwa mikononi mwa polisi huku akiwa ni marehemu na cha kushangaza maiti hiyo ilizikwa na polisi kutokana na kutotambulika kwa mara moja’’.

Baada ya kusikia hivyo kuwa kuna mtu amezikwa na jeshi la polisi kutokana na kutotambulika kwa ndugu zake ilibidi waende kuangalia ndipo polisi iliwaonesha nguo ambazo alikuwa amevaa hapo ndipo alipogundulika kuwa ni yeye .

Aliendelea kuelezea mkasa huo Kijana huyo alisema ,Mdogo wangu tumetafuta sana kwa kushirikiana na jeshi la polisi bila ya mafanikio na ndipo tuliamua kwenda kwa Mganga wa kienyeji ili tujue mahali alipo ni salama na ni sehemu gani.

‘’Nilikwenda kwa Mganga huyokatika kijiji cha Chimbuya ambacho kipo katika Wilaya ya Momba mkoani hapa,Mganga hakutoa majibu ya mahali ambapo yupo ila aliniambia kuwa yupo hai ila ni kukazana tu kumtafuta na hupo hapa hapa Tanzania.

Mara baada ya mganga huyo nilikwenda kwa mganga mwingine katika kijiji cha Anseketwa kilichopo katika Wilaya hii ambaye anasema kuwa walishindana kutokana na mashart aliyompa ya kukata kidole chake cha mwisho katika mkono wa kushoto ili kuipa mizimu yake nyama.
Mdogo wa Nzito
Kijana huyo aliendelea kueleza kwamba baada ya mimi kuona hivyo niliamua kukataa mashart ndipo mganga alinitoza faini ya shilling laki mbili huku akisema kuwa atachukuwa kwa muda wake pesa hizo mpaka atakapo maliza deni lake,

Aliongeza kuwa  baada ya maneno ya Mganga nilitoka na kurudi nyumbani mara baada ya kufika nyumbani  kuna pesa nilikuwa nazo nikakuta hazipo ghafla ukatokea mzimu ambao uliniambia kuwa si nilikwambia kuwa nitachukuwa kwa muda wangu sasa ndo nimechukuwa ukapotea.

‘’Kutokana na hile hali ya kutokewa na mzimu niliamua kuacha kwenda kwa waganga wa kienyeji mara baada ya mzimu huo kutaka kumzuru kwa kukataa shart ambalo aliambiwa na Mganga juu ya kuchangia mashetani yake ndipo yamsaidie kumwonyesha.

Pia ,alisema pamoja na mdogo wangu kuto kuaga kwa rafiki yake yeyote hapo ndio panapo umiza kichwa sana na kusababisha nyumbani kuwe kama kuna msiba hivyo basi kwa yeyote ambaye atakuwa anafahamu alipo  au alishawahi kumuona sehemu yeyote apige simu no 0757162769

Je, Una Habari,Picha,Tangazo,Makala, Ushauri n.k.?Basi Wasiliana Nasi Simu/WhatsApp 0759 406 070

Post a Comment

 
Top