Share this PostPin ThisShare on TumblrShare on Google PlusEmail This

Afisa Elimu Shule za msingi Jiji la Mbeya,Auleria Lwenza wa kwanza kulia akikagua baadhi ya maeneo ya shule ya msingi Ilemi ambayo imekumbwa na janga la kuizuliwa paa zake na mvua kubwa iliyonyesha ambayo iliambatana na upepo mkali feb 20 mwaka huu.
Moja ya Vyumba vya madarasa vilivyo athiriwa vibaya na mvua hizo.





Wakazi wa eneo la  Ilemi jijini Mbeya wakiwa juu ya paa za nyumba zao wakijaribu kufanya ukabati mdogo baada ya nyumba zao kuharibiwa na mvua iliyoambatana na upepo mkali












Mwanafunzi wa shule ya msingi Ilemi Darasa  la Tano ambaye aliangukiwa na ukuta akipelekwa hospital kwa matibabu zaidi.
                                      (Picha na Fahari News)


Mvua za masika zinazoendelea kunyesha nchini Tanzania leo hii zimezua balaa baada ya mvua kubwa iliyoambatana upepo mkali kunyesha katika maeneo mbalimbali jijini Mbeya na kuleta maafa. Kati ya maeneo yaliyoathiriwa na mvua hiyo ni pamoja na Ilemi jijini Mbeya ambapo takribani kaya 40 pamoja na shule zimeezuliwa, huku wanafunzi wawili wa shule ya msingi Ilemi wakijeruhiwa kwa kuangukiwa na kuta za shule hiyo.

Mashuhuda wa mvua hiyo iliyonyesha kwa karibu dakika 20 mchana majira ya saa nane wameeleza kuwa mvua hiyo iliambatana na upepo mkali ambao uliweza kuangusha kuta pamoja na miti na kuhatarisha maisha ya wakazi wa maeneo hayo. Kuhusiana na shule zilizoathiriwa na balaa hilo, Vyumba vya madarasa, ofisi na vyoo vimeezuliwa na upepo na baadhi ya kuta kudondoka ambapo Afisa Elimu jiji la Mbeya kwa shule za msingi, Auleria Lwensa msingi ambaye alifika katika eneo la tukio amewataka waalimu na wanafunzi kuendelea kuyatumia madarasa na ofisi ambayo hayajaathiriwa.

 Pamoja na hayo bi. Auleria amesema kuwa shule haitafungwa na badala yake masomo yataendelea huku ukifanywa utaratibu na bodi ya shule ili kuwezesha ukarabati wa majengo hayo huku akiwataka wakazi wa maeneo hayo kupeana msaada unaowezekana kwa zile familia zilizoathirika na janga hilo kwakuwa ni jambo la dharura.





Je, Una Habari,Picha,Tangazo,Makala, Ushauri n.k.?Basi Wasiliana Nasi Simu/WhatsApp 0759 406 070

Post a Comment

 
Top