February 15, 2025 01:56:22 PM Menu

Share this PostPin ThisShare on TumblrShare on Google PlusEmail This

Timu ya Mwadui kutoka mjini Shinyanga jana imetawazwa kuwa Mabingwa wapya wa Ligi Daraja la Kwanza (FDL) baada ya kuifunga timu ya African Sports ya jijini Tanga kwa bao 1 - 0, katika mchezo uliofanyika Uwanja wa Azam Comlex Chamazi jijni Dar es alaam.
Bao pekee na la ushindi kwa timu ya Mwadui lilifungwa na mshambulaji Kelvin Sabato Kongwe dakika ya 53 ya mchezo na kuihakikishia Mwadui ushindi katika mchezo huo wa fainali.
Mabingwa hao wapya wa Ligi Daraja la Kwanza (FDL) walizawadia Kombe la Ubingwa, medali pamoja na hundi ya sh.millioni tatu, huku timu ya African Sports ikipata medali na hundi ya sh. millioni 2.
Shirikisho la Mpira wa Miguu nchini TFF linaipongeza timu ya Mwadui kwa kuibuka Bingwa mpya wa Ligi Daraja la Kwanza (FDL) msimu wa 2014/205.
Jumla ya timu nne zimepanda Ligi Kuu msimu ujao ambazo ni  Bingwa Mwadui FC, African Sports, Majimaji na Toto Africans.
MWISHO.

Je, Una Habari,Picha,Tangazo,Makala, Ushauri n.k.?Basi Wasiliana Nasi Simu/WhatsApp 0759 406 070

23 Feb 2015

Post a Comment

:) :)) ;(( :-) =)) ;( ;-( :d :-d @-) :p :o :>) (o) [-( :-? (p) :-s (m) 8-) :-t :-b b-( :-# =p~ $-) (b) (f) x-) (k) (h) (c) cheer
Click to see the code!
To insert emoticon you must added at least one space before the code.

 
Top