Na Emanuel Madafa,Mbeya
Waziri Mkuu Mheshimiwa Mizengo Pinda anatarajiwa kuanza ziara ya kikazi ya siku Nane Mkoa wa Mbeya ambayo itahusisha Halmashauri saba za Mkoa huo.
Katika ziara hiyo Mheshimiwa
Waziri Mkuu atatembelea halmashauri Saba za Mkoa huo ambazo ni Halmashauri ya jiji la
Mbeya ,Kyela,Busokelo Rungwe ,Mbozi pamoja na Chunya kuaznia Feb 23 hadi Machi 1 mwaka huu..
Akizungumza jijini mbeya Mkuu
wa Mkoa wa Mbeya Abbas Kandoro amesema Lengo la Ziara hiyo ni kukagua
miradi mbalimbali ya maendeleo
inayotekelezwa na serikali halmashauri
pamoja na wadau mbalimbali wa maendeleo katika mkoa wa mbeya.
Amesema katika Ziara hiyo Waziri Pinda atakagua na kuweka mawe ya msingi pamoja na kuzindua
miradi katika sekta ya Elimu ,Afya ,Ujenzi Barabara kilimo na umwagiliaji maji
masoko na hifadhi ya chakula.
Aidha amesema Waziri Mkuu atapata fursa ya kuhutubia
mikutano ya hadhara ambayo itafanyika katika kila Halmashauri husika katika
ziara hiyo.
Pia amewataka wananchi wa
mkoa wa mbeya kuendelea kudumisha amani na utulivu katika siku zote Nane za ziara ya Waziri Mkuu ambapo
amewahakikishia wananchi kuwa serikali imejipanga vyema katika kuhakikisha mkoa
unakuwa salama katika kipindi hicho.
Mwisho..







Post a Comment