Meneja
wa Mauzo kampuni ya Mohamed Enterprises .Co.ltd tawi la mbeya Ndugu Peter
Mkumbukwa (37) mkazi wa mbeya amefariki dunia baada ya gari walilokuwa
wakisafiria lenye namba za usajili T.784
Dca aina ya shandon lililokuwa likiendeshwa na dereva aitwaye Juma Alukamba kuligonga kwa nyuma gari T.928 CKK aina ya fuso. likiendeshwa na
dereva lifu mahenge.
Ajali
hiyo ilitokea Machi 25 ,2015 majira ya saa 8 mchana huko katika
eneo la kijiji cha Idweli, kata ya isongole, , wilaya ya rungwe, mkoa wa mbeya
katika barabara kuu ya mbeya/tukuyu.
Kamanda
wa Polisi Mkoa wa Mbeya Ahmed Msangi amesema katika ajali hiyo, dereva wa gari lenye namba T.784 DCA Juma Alukamba alijeruhiwa na amelazwa katika hospitali ya misheni Igogwe.
Amesema chanzo
cha ajali hiyo ni mwendo kasi wa gari namba T.784
dca ambapo mara baada ya jail hiyo Dereva wa fuso alikimbia, huku juhudi za kumtafuta
zinaendelea.
Aidha
Msangi anatoa wito kwa madereva kuwa makini
wanapotumia vyombo vya moto ikiwa ni pamoja na kuzingatia sheria/kanuni na
alama za usalama barabarani ili kuepuka ajali zinazoweza kuepukika.
MWISHO







Post a Comment