Share this PostPin ThisShare on TumblrShare on Google PlusEmail This
Marion Suge Knigh
Mahakama kuu imemuachilia kwa dhamana ya dola millioni 25 msanii wa muziki wa rap Suge Knight ,ambaye anatuhumiwa kwa kuwagonga wanaume wawili katika eneo la Campton nchini Marekani ,na kumuua mmoja.
Mda mfupi baada ya kusikizwa kwa kesi yake msanii huyo mwenye umri wa miaka 49 alianguka na kuzirai mahakamani ,ikiwa ni mara ya tatu kwa yeye kupelekwa hospitalini kufuatia kusikizwa kwa kesi yake.
Wakili wake alisema kuwa macho ya mteja wake yalianza kucheza cheza kabla ya kuanza kutokwa na jesho na mwishowe kuanguka huku akigonga kichwa chake katika meza na kupoteza fahamu.
Knight anatarajiwa kurudi mahakamani mwezi Aprili 13 ambayo ni siku ya kusikilizwa kwa kesi yake.
Katika kusikizwa kwa ombi la kutaka kuwachiliwa kwa dhamana, Suge Knight alishtumiwa kuwa muhalifu asiyetubu.

Je, Una Habari,Picha,Tangazo,Makala, Ushauri n.k.?Basi Wasiliana Nasi Simu/WhatsApp 0759 406 070

Post a Comment

 
Top