Share this PostPin ThisShare on TumblrShare on Google PlusEmail This
PICHA MAKTABA


Na Mwandishi wetu,Mbeya  ,Mbeya
Watu 15 wamenusurika kifo baada ya gari walilokuwa wakisafiria  mali ya Kampuni ya Taqwa Lenye Namba za Usajili T.791 Bzr aina Ya Nissan Lililokuwa likiendeshwa na  Salumu Selemani (45) Mkazi Wa D’salaam Kuligonga gari namba za usajili  T.778 Can Isuzu Ftr likiendeshwa na Edwin Luyenga (40)

Ajali Hiyo Imetokea Mei 10 mwaka huu Majira ya Saa  2 usiku   Katika Kijiji cha Kapyo, Kata ya Mahongole, , Wilaya ya Mbarali, Mkoa Wa Mbeya Katika Barabara Kuu Ya Mbeya/Njombe.

Kaimu Kamanda wa Polisi Mkoa wa mbeya Nyigesa Wankyo amewataja baadhi ya majeruhi katika ajali hiyo kuwa ni Apamat Umuyu (41) Mkongo raia wa nchini Kongo , Salumu Rashidi (29) Mkazi Wa Dsm ,Juma Rajabu (34) Mkazi wa Zanzibar ,Anna Misikita (36) Mkongo , David Mtachi (43) Mkazi Wa Dsm , Groli Amani (41) Mkazi Wa Dsm , Kelvin Jordan (39) Mkazi Wa Dsm.

Majeruhi Wengine ni  Lika Ilunga (47) Mkazi Wa Kongo . Majariwa Ramadhani (51) Mkazi Wa Kagera 12. Adela Mutomba (46) Mkazi Wa Kongo , Mudy Abdallah (43) Mkazi Bukoba, Nasoro Mkazi wa Tanga. Ambapo wengine wamekwisha tibiwa na kupatiwa luhusa katika hospital ya Rufaa Mbeya ambapo chanzo cha hiyo ni mwendokasi wa dereva wa basi hilo..

Kaimu Kamanda Wa Polisi Mkoa Wa Mbeya Kamishna Msaidizi Wa Polisi Nyigesa  Wankyo ametoa  Wito Kwa Madereva Kuwa Makini Wanapotumia vyombo vya moto ikiwa ni pamoja na kufuata sheria za usalama barabarani .
Mwisho.

Je, Una Habari,Picha,Tangazo,Makala, Ushauri n.k.?Basi Wasiliana Nasi Simu/WhatsApp 0759 406 070

Post a Comment

 
Top