Share this PostPin ThisShare on TumblrShare on Google PlusEmail This
Mkurugenzi  wa masoko utafiti  na huduma  kwa wateja Bi.Tully Mwambapa aliyemwakilisha  mkurugenzi mtendaji wa Benki  ya CRDB  akimkabidhi funguo ya gari  mshindi wa gari aina ya paso Ndugu . Mwinyi Hamis Juma,baada ya kushinda shindano la Tuma pesa na simbanking Shinda Paso hafla ambayo  iliyofanyika June 16  katika tawi la Mwanjelwa, Jijini hapa. 


Mshindi wa gari akiwa katika gari lake


Wafanyakazi wa benki ya CRDB pamoja na wateja mbalimbali wa benki hiyo wakiwa katika hafla ya utoaji wa zawadi kwa mshindi wa shindano la Tuma Pesa na Simbanking Shinda Passo nje ya ofisi za Benki hiyo Mwanjelwa jijini Mbeya June 16 mwaka huu,PICHA Jamiimojablog.




Mshindi katika picha ya pamoja na Mkurugenzi  wa masoko utafiti  na huduma  kwa wateja Bi.Tully Mwambapa pamoja na baadhi ya maofisa wa benki ya CRDB Tawi la Mwanjlewa jijini Mbeya



Mkurugenzi  wa masoko utafiti  na huduma  kwa wateja Bi.Tully Mwambapa akizungumza katika hafla hiyo.


Mkurugenzi  wa masoko utafiti  na huduma  kwa wateja Bi.Tully Mwambapa akiwa akizungumza jambo katika sherehe za siku ya Mtoto wa Afrika ambayo ilijumuisha  wafanyakazi wa benki hiyo pamoja na  watoto zaidi ya 50 walioletwa na wazazi wao kwa ajili ya kuwafungulia akaunti ya Jumbo Junior.






Benki ya CRDB leo imekabidhi zawadi  ya gari aina ya Passo   mshindi wa shindano  la tuma pesa na simbanking shinda passo  kwa mfanyabiashara kutoka Zanzibar ambaye hufanya biashara zake jijini mbeya Ndugu Mwinyi Hamisi  ikiwa ni gari ya pili kutolewa toka kuanza kwa shindano hilo.



Akikabidhi gari hilo kwa niaba ya Mkurugenzi Mkuu, Dk. Charles Kimei, katika hafla fupi iliyo fanyika katika benki CRDB Tawi la Mwanjelwa Mkurugenzi Masoko Utafiti na Huduma kwa Wateja, Tully Mwambapa, amesema promosheni hiyo ni moja ya mikakati  iliyojiwekea Benki ya CRDB katika kuhakikisha inaongeza chachu na kukuza uchumi kwa wateja wao .

.

Amesema kupitia  huduma    ya SIMBANK  mteja anaweza kushinda zawaidi hiyo ya gari kwa kutuma pesa au kutoa pesa kupitia huduma ya simu ambapo moja kwa moja ataingizwa katika promosheni hiyo .



Kutokana na shindano hilo amesema kuwa  vijana wanapaswa  kuachana  na matumizi mabaya ya simu  ambayo yamekuwa  yakiwaingiza katika  maovu na hivyo waitumie  huduma  hiyo kwa ajili ya kuwawezesha  kupata  huduma  bora na  ya haraka yenye usalama mkubwa  sanjali na kupata  zawadi nyingi.



Amesema, wanatambua changamoto zilizopo ndani ya jamii na kwamba serikali pekee haiwezi kuzitatua, hivyo  wao kupitia huduma za kibenki  wameamua kuanzisha shindano hilo ili kuwapa motisha zaidi wateja wao.



Aidha, Sherehe hiyo iliyoenda sanjari na sherehe za siku ya Mtoto wa Afrika , wafanyakazi wa benki hiyo walitumia fursa hiyo kuburudika na watoto zaidi ya 50 walioletwa na wazazi wao kwa ajili ya kuwafungulia akaunti ya Jumbo Junior.



Akizungumzia akaunti hiyo maalumu kwa watoto Mkurugenzi huyo wa masoko alisema akaunti hiyo ni nguzo kubwa kwa maendeleo ya watoto,

 kwani kupitia akaunti hiyo wazazi wanaweza kuwa na uhakika wa kutimiza malengo ya kielemu kwa watoto wao


Naye  mshindi huyo baada ya kukabidhiwa funguo ya gari hilo lenye thamani ya shilingi Milioni 12, alisema amefurahi sana kwa kushinda zawadi ya gari kutoka CRDB kwani imembadilishia mfumo wa maisha yake.





Aidha ametoa wito kwa jamii kuacha tabia ya kumiliki simu kubwa pasipo kuwa na malengo ya aina yeyote badala yake watumie kujifunza mambo mbalimbali hususani katika suala la kufahamu masoko   na namna ya kupanua biashara zao.

Mwisho

Je, Una Habari,Picha,Tangazo,Makala, Ushauri n.k.?Basi Wasiliana Nasi Simu/WhatsApp 0759 406 070

Post a Comment

 
Top