Share this PostPin ThisShare on TumblrShare on Google PlusEmail This



MTOTO  wa muasisi wa Taifa la Tanzania, Baba wa Taifa, Hayati Mwalimu Julius Kambarange Nyerere, Makongoro Nyerere, akizungumza na wananchama wa chama cha mapinmduzi ccm jijini mbeya wakati akiomba kupata udhamini kwa wanachama hao.a
Wanachama wakimsikiliza Makongoro












MTOTO  wa muasisi wa Taifa la Tanzania, Baba wa Taifa, Hayati Mwalimu Julius Kambarange Nyerere, Makongoro Nyerere, amesema amewataka watanzania  kuumpa ridhaa ya kupeperusha bendera ya chama cha mapinduzi ccm ili aweze kurudisha heshima ya chama hicho katika uchaguzi mkuu ujao mwezi octoba .





Makongoro, amesema hayo , wakati wa zoezi la kuwapata wadhamini watakao mdhamini nafasi ya urais ambapo katika zoezi hilo zaidi ya mamia ya wanachama wa Chama Cha Mapinduzi CCM, na wakazi wengine wa Mkoa wa Mbeya, jana Jumatatu  Juni 8, 2015, walifurika kwa wingi kwenye ofisi za CCM Mkoa wa Mbeya,na kumdhamini kiongozi huyo.




Akizungumza na umati huo mkubwa  katika ukumbi wa ccm jijini mbeya , Makongoro aliwataka wakazi wa Mkoa wa Mbeya kuhakikisha wanamuunga mkono wa kumchagua kuwa rais na kuachana na wagombea ambao wameonekana kutokuwa watiifu na waadilifu kwa  chama na Taifa  kwa ujumla hali ambayo imechangia kwa kiwango kikubwa chama hicho kupoteza mvuto wako .




Aidha, Makongoro  amesema  kuwa chama cha mapinduzi kimekuwa kikiongozwa na taratibu zake ambazo zinapaswa kufuata na wananchama wote.



Amesema waasisi wa chama hicho ambao ni hayati baba wa Taifa Mwalimu Julias nyerere walikiacha chama hicho katika mstari mzuri hali ambayo kwa sasa imekuwa tofauti hivyo  kuna haja ya kufanya mabadiliko kwa kuhakikisha hali hiyo inalejea kama kawaida.



Mwisho.

Je, Una Habari,Picha,Tangazo,Makala, Ushauri n.k.?Basi Wasiliana Nasi Simu/WhatsApp 0759 406 070

Post a Comment

 
Top