Share this PostPin ThisShare on TumblrShare on Google PlusEmail This
Afisa Mahusiano Mamlaka ya maji safi na usafi wa Mazingira jijini Mbeya (Uwsa)Neema Stantony


Na Mwandishi wetu,Mbeya 

Mamlaka Maji Safi na Usafi wa Mazingira jijini Mbeya  (UWSA)imeamua kuboresha mfumo wa huduma za ulipaji wa ankara za maji kwa wateja wake  kwa kutumia huduma za  M-pesa,Tigo Pesa pamoja na mitandao mingine ikiwa na lengo la kuongeza idadi ya walipaji wa huduma hiyo sanjali na kuondoa adha kwa wateja wao.


Akizungumza jijini Mbeya Afisa mahusiano Mamlaka ya Maji safi na usafi wa Mazingira (Uwsa) Ndugu Neema Stantony amesema mfumo wa ulipaji wa huduma za maji kupitia mitandao hiyo ya simu umeleta  urahisi wa malipo ya huduma ya maji  mahala popote pale nchini.


Amesema  hatua hiyo mpya imechangia kwa kiasi kikubwa kuleta huduma bora kwa wakazi wa mji wa Mbeya katika viwango vya juu zaidi.


Amesema mara badaa ya kaunzisha huduma hiyo mwitiko umekuwa mkubwa sana hasa kutokana na kupungua kwa foleni wakati wa ulipaji wa Ankara hizo sanjali na kuwepo kwa ongezko kubwa la watu kulipa Ankara zao.

Amesema mfumo huo umeondoa  usumbufu wa kutumia muda mrefu kwenye foleni za kulipia huduma ya maji nakwamba huduma  hiyo  ni hatua ya kipekee hasa ikizingatiwa kuwa badala ya kupoteza muda kukaa foleni mteja anaweza kuendelea na shughuli zake za kila siku.

Aidha Neema amesema changamoto kubwa iliyopo kwa sasa ni kwa baadhi ya wateja kulipa Ankara zao za maji katika mamlaka  nyingine za maji kama Dawsco hivyo kuletea usumbufu wakati wa ufuatiliaji.

Amesema hali hiyo pia  inatokana na baadhi yao kusahau akaunti zao  sanjali na kutokuwa makini wakati wa ulipaji wa huduma hiyo.

Wakati huo huo Afisa huyo amewaondoa hofu nwakazi wa jiji la mbeya ambao wanapata huduma ya maji kwa muda mfupi kuwa suala hilo linatokana na kuhalibiwa kwa miundombinu ya maji hasa kwa maeneo ambayo kunafanyika matengenezo ya barabara.JAMIIMOJABLOG



 Mwisho.


Je, Una Habari,Picha,Tangazo,Makala, Ushauri n.k.?Basi Wasiliana Nasi Simu/WhatsApp 0759 406 070

Post a Comment

 
Top