Kikosi
cha timu ya Taifa ya vijana umri chini ya miaka 15 (U-15) kitaingia
kambini siku ya jumatatu tarehe 22/06/2015 ili kujiandaa na mchezo wa
kirafiki dhidi ya kombaini ya mkoa wa Mbeya, mchezo utakaofanyika mjini
Mbeya jumatatu ya tarehe 28/06/2015.
Kikosi
hiki kinaandaliwa kwa ajili ya kujiandaa na na michuano ya mtoano
kuwania kufuzu kwa fainali za Afrika kwa vijana wenye umri chini ya
miaka 17 zitakazofanyia nchini Madagascar mwaka 2017. Hatua ya mtoano wa
awali itaanza mwakani 2016 mwezi Juni.
Timu
itakua chini ya kocha Bakari Shime kwa muda akisaidiwa na Peter
Manyika. Kocha aliyekua ameteuliwa awali kufundisha timu hiyo Adolf
Rishard ameomba udhuru baada ya kupata fursa ya kwenda masomoni.
Wachezaji
watakaoingia kambini na mikoa wanayotokea kwenye mabano ni Mwijuma
Yahya (Tanga), David Mpakazi, Shilole Anthony (Geita), Kibwana Shomari ,
Ibrahim Koba, (Morogoro), Faraji John, Kelvin Deogratius, Davison Meddy
, Maulid Lembe (Dodoma), Ally Msengi (Mwanza).
Wengine
ni Timoth Timothy, Juma Juma, Pius Raphael, Mohamed Ally (Dodoma),
Athumani Rajabu, Juma Zubeir, Jonathan Rafael (Kigoma), Robert Philip,
Jaffari Juma (Arusha), Michael Kanuti, Alex Peter, Rashid Kilongola
(Kinondoni), Morris Michael (Ilala), Karim Mfaume (Lindi), Assad Juma
(Unguja Magharibi), Francis Mrope, Kelvin Pius (Mara)
IMETOLEWA NA SHIRIKISHO LA MPIRA WA MIGUU TANZANIA (TFF)







Post a Comment