Na Frank Shija, WHVUM
Bodi
ya Filamu Tanzania imepongeza kwa juhudi zake za kuendeleza na kusaidia
kukua kwa tasnia ya filamu nchini.
Pongezi hizo zimetolewa juzi jijini Dar es Salaam na Balozi Paul Rupia
alipokuwa mgeni rasmi katika hafla ya uzinduzi wa Filamu ya Desire to
Succeed.
Balozi
Rupia alisema kuwa tasnia ya filamu inazid kukua nchini sambamba na
kuongezeka kwa wasanii kuzingatia maadili ya Kitanzania.
"Niseme
wazi tu kwamba Serikali kupitia Bodi ya Filamu nchini inafanya kazi
thabiti tofauti na ilivyokuwa huko nyuma ambapo watendaji wa Bodi hiyo
walikuwa na kazi ya kukagua tu tofauti na sasa wanatoka na kuhamasisha
ukuaji wa tasnia hii” Alisema Balozi Rupia.
Aidha
Balozi Rupia ametoa rai kwa taasisi za umma na binafsi kutambua mchango
wa wasanii na kuwatumia vyema katika program zao za kujitangaza ndani na
nje ya nchi kama ambayvo DCB benki ilivyotumia fursa hiyo.
Kwa
upande wake Mwakilishi wa Kampuni ya Consnet Group Bw. Sanctus Mtsimbe
amesema kuwa imekuwa ni faraja kwa wasanii kuona kuwa kazi zao na
mchango wao katika jamii unatambuliwa na baadhi ya taasisi hapa nchini
na kuongeza kuwa hiyo inaonyesha dalili njema katika ukuaji wa tasnia ya
filamu.
Aliongeza
kuwa katika filamu ya hiyo ya Desire to Succeed wasanii wameitendea
haki kazi yao na kwa kuzingatia matakwa ya kanuni na maelekezo ya Bodi
ya Filamu Tanzania ikiwa ni pamoja na kuzingatia mavazi yenye staha kwa
mujibu wa maadili ya kitanzania.
Mtsimbe
ametoa rai kwa wadau wa tasnia ya filamu kununua nakala za filamu hiyo
ambayo itapatikana madukani kwa bei ya shilingi 3000/= ili wajionee
namna kazi nzuri ya wasinii wetu.
Filamu ya Desire to Suicceed ni filamu ya kwanza nchini Tanzania ambayo
maudhui yake yamekuwa na malengo makuu mawili kwa wakati mmoja ikiwa ni
kuelimisha na matangazo ya biashara kwa wahusika kutumia Bidhaa za Benki
ya DCB katika kuuisha hadithi yao. DCB Benki ndiyo mdhamini wa filamu
hiyo ambaoyo imetengenezwa na Kapmuni ya Consnet Group huku
ikishirikishwa wasanii Tito Mrisho Zimbwe (Muhusika Mkuu), Rose
Ndauka,Jackline Pentezel, Hidaya Njiadi, Gojak na wengine.
Kutoka kushoto ni Katibu Mtendaji wa Bodi ya Filamu
Tanzania Bibi. Joyce Fissoo, msanii Rose Ndauka, Tito Mrisho Zimbwe na
Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi wa Benki ya Biashara ya DCB Balozi Paul Rupia
wakionyesha DVD ya filamu ya Desire to Succeed juzi jijini Dar es Salaam mara baada
ya kuzinduliwa rasmi. Filamu hiyo imetengezwa na kampuni ya Consnet Group chini
ya udhamini wa DCB Benki ikiwa ni njia ya kujitangaza kupitia ubunifu wa sanaa
ya filamu.
Post a Comment