Share this PostPin ThisShare on TumblrShare on Google PlusEmail This
WAZIRI wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa na Mbunge wa Jimbo la Mtama, Bernard Membe akiwasalimu wanaccm na wananchi wa jiji la mbeya mara baada ya kuwasili kwa lengo la kupata  wadhamini katika ofisi za ccm sokomatola jijini mbeya .







WAZIRI wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa na Mbunge wa Jimbo la Mtama, Bernard Membe akizungumza na wanachama wa ccm mkoa wa mbeya ambao walijitkeza kwa lengo la kumdhamini.









Heka heka na kuelekea katika uchaguzi mkuu mwezi octoba umezidi kupamba moto ambapo kwa Chama Cha Mapinduzi (CCM) makada mbalimbali waliotangaza nia ya kuwania nafasi ya urais kupitia chama hicho wameendelea na mchakato wa kutafuta wadhimi katika mikoa 15 ya Tanzania bara na Zanzibar  katika kutekeleza taratibu zilizowekwa na chama hicho.
Hadi sasa katika mkoa wa mbeya  makada watatu wamekwisha kamilisha zoezi hilo la kutafuta wadhamini ambao ni Waziri wa Uchukuzi Samwel Sitta ,Mtoto wa hayati  mwalimu nyerere Makongoro pamoja na Waziri wa Mambo ya nje na Ushirikinao wa kimataifa  Bernard Membe ambapo kila mmoja alitumia nafasi hiyo kujinadi na kumwaga sera zake  .
Hii leo June 10 WAZIRI wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa na Mbunge wa Jimbo la Mtama, Bernard Membe, amesema endapo Kamati kuu ya CCM haitalipitisha jina lake katika kuwania nafasi ya kuteuliwa kugombea nafasi ya urais kwa mwaka 2015, kura yake ataipeleka kwa mgombea Marck Mwondosya.
Amesema, miongoni mwa wagombea wote waliotangaza nia yakuwania kuteuliwa kugombea nafasi ya urais kupitia chama cha mapinduzi CCM ni wagombea wawili tu akiwemo yeye na  Mark Mwandosya ambao wameweza kukidhi vigezo vya kuliongoza Taifa hili.
Akizungumza, wakati wa zoezi la kuwapata wadhamini watakao mdhamini nafasi ya urais ambapo katika zoezi hilo zaidi ya mamia ya wanachama wa Chama Cha Mapinduzi CCM, na wakazi wengine wa Mkoa wa Mbeya, walifurika kwa wingi kwenye ofisi za CCM Mkoa wa Mbeya,na kumdhamini kiongozi huyo.

 Amesema, kama asipo pitishwa yeye yupo tayari kukaa chini kumpisha Mwandosya kwani ni kiongozi shupavu na muadilifu na amejaliwa kuwa na kila dhamana ya kuliongoza Taifa la Tanzania.

 Aidha, Membe aliwataka wakazi wa Mkoa wa Mbeya, kuhakikisha wanayapitisha majina mawili ya wagombea wa nafasi za urais likiwemo jina lake na la Mark Mwondosya.

Mwisho.

Je, Una Habari,Picha,Tangazo,Makala, Ushauri n.k.?Basi Wasiliana Nasi Simu/WhatsApp 0759 406 070

Post a Comment

 
Top