Share this PostPin ThisShare on TumblrShare on Google PlusEmail This
Zaidi ya watu 90 wamefariki kutokana na pombe iliokuwa na sumu katika mji wa India, Mumbai huku wengi wengine wakiwa hospitalini.
Vifo vya kwanza viliripotiwa siku ya jumatano.
Naibu wa kamishna wa polisi katika mji huo amesema kuwa watu 150 waliokunywa pombe hiyo iliotengezwa nyumbani katika mtaa mmoja wa mabanda.
Vifo vinavyosababishwa na pombe ilio na sumu vimekuwa jambo la kawaida nchini India ambapo pombe rahisi inayotengezwa nyumbani ni maarufu miongoni mwa wakaazi wake walio maskini.

Je, Una Habari,Picha,Tangazo,Makala, Ushauri n.k.?Basi Wasiliana Nasi Simu/WhatsApp 0759 406 070

Post a Comment

 
Top