Share this PostPin ThisShare on TumblrShare on Google PlusEmail This
Meneja msaidizi wa bidhaa za Zuku Tanzania, Venaranda Raphael, amezitaka kampuni zinazofanya shughuli za filamu nchni zizingatie maadili kwa kuonyesha filamu zao usiku ili zisiharibu taibia za watoto walio chini ya umri  wa miala 18.
Alisema filamu nyingi zina picha zisizofaa kwa  watoto hivyo zionyeshwe usiku wa manane ambapo inaaminika  kwamba muda huo idadi kubwa ya watoto huwa wamelala.
Naye memeja mkuu wa kampuni hiyo, Omari Zuberi, alisema kampuni hiyo imewekeza dola milioni moja kwa kipindi cha miaka 10 ili kusaidia  Tamasha la Filamu Zanzibar (ZIFF) kupata  watu wenye vipaji ndani na nje ya nchi.
Katika tamasha hilo, filamu zitakazoshindandishwa  katika kipengele cha ‘Zuku Bongo Movies’ ni Mapenzi ya Mungu,Mr.Kadamanja, Fundi Seremala, Daddy’s Wedding, VIP, Single Zero,Kutakapokucha,Msago, Mikono Salama na Nyange Kigoma.
Nyingine ni Mbawa Mwitu, Samaki Mchangani,Faraja, Pichu, Going Bongo na Kilimo 2.
Hata hivyo mkurugenzi  wa Tamasha hilo, Prof.Martin Mhando  alisema kwa pamoja ZIFF na Zuku wanasaidia  kuendeleza tasnia yafilamu  za bongo  kwa kuwa wanathamini sanaa ndiyo maana wanaamini kwamba itasaidia kuwaongezea ujuzi watayarishaji wa filamu zakiswahili kwa kuwa hitaji la filamu zao ni kubwa.
Mtanzania

Je, Una Habari,Picha,Tangazo,Makala, Ushauri n.k.?Basi Wasiliana Nasi Simu/WhatsApp 0759 406 070

Post a Comment

 
Top