Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mbeya Ahmed Msangi |
Mbeya
Watu wanaosadikiwa kuwa ni majambazi wavamia na
kujeruhi na kisha kupora mali mbalimbali baada ya kuweka kizuizi cha mawe na magogo
katika barabara ya mbalizi-mkwajuni.
Tukio hilo limetokea usiku wa kuamkia leo majira ya saa 02:00 huko eneo la
msitu wa mlima msangamwelu, kijiji cha mjele, kata ya mshewe, , wilaya ya mbeya
vijijini, mkoa wa mbeya.
Aidha katika tukio hilo wahanga hao ambao walikuwa
wanakwenda galula kuhudhuria sherehe ya upadrisho, waliporwa pesa taslimu
ambazo bado kufahamika kiasi gani, mabegi ya nguo mbalimbali, zawadi za
waumini, simu za mikononi pamoja na
majoho. Wahanga wamepatiwa matibabu na
kuruhusiwa.
Kwa mujibu wa Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mbeya Ndugu
Ahmed Msangi amesema kuwa watu
hao ambao majina yao hayakufahamika mara moja ambao wanasadikiwa kuwa
majambazi walitumia mbinu ya kuliwekea
vizuizi gari lenye namba za usajili Sm
3496 aina ya toyota land cruiser mali ya hospitali ya mwambani chunya
lililokuwa likiendeshwa na dereva loved
mwandongo (53) mkazi wa mkwajuni.
Aidha gari hiyo hiyo ilikuwa imebeba mapadri watatu wanafunzi ambao ni ambao ni Furaha Henjewele (36)Mkazi wa Mbeya alipigwa fimbo kichwani na kukatwa panga mkono
wa kulia.
Wengine ni pamoja na Padri Gasper Mwashimwanga (37) mkazi wa mpuguso – tukuyu Henry Mwalyanga (33) Eliakim kasegila (27)
mkazi wa peramiho na Padri bonifasi chalo (46) mkazi wa mwanjelwa.
Msako mkali unaendelea ili kuwabaini waliohusika
katika tukio hili ili wakamatwe na hatua za kisheria zichukuliwe dhidi yao
mwisho
Post a Comment