KAMATI
ya Kudumu ya Bunge imeitaka serikali kuhakikisha inatoa fedha za mradi
wa ujenzi wa jengo la abiria namba tatu (terminal III) kwa wakati ili
mradi huo uweze kukamilika kama ilivyopangwa.
Mwenyekiti
wa kamati hiyo, Profesa Norman Sigalla aliyasema hayo wakati wa kufanya
majumuisho baada ya kutembelea mradi huo leo katika Uwanja wa Ndege wa
Kimataifa wa Julius Nyerere (JNIA).
Alisema
kukamilika kwa jengo hilo kwa wakati uliopangwa utawapa heshima
Watanzania lakini pia kupunguza msongamano katika jengo la sasa la
Terminal II.
“Nchi
inapoenda kwa sasa ni kuzuri, lakini ili kukamilika ujenzi huu kwa
wakati tunaomba serikali itoe fedha ili kufanikisha hilo, baada ya
kukamilika kila ndege itatua hapa nchini na hivyo kuongeza pato la
Taifa,” alisema Profesa Sigalla.
Awali
Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa mamlaka ya Viwanja vya Ndege (TAA), Salim
Msangi alisema, miongoni mwa changamoto wanazokumbana nazo katika
utekelezaji wa mradi huo ni serikali kutotoa fedha kwa wakati pamoja na
sheria ya Mamlaka ya Mapato (TRA) ya kodi ya Ongezeko la Thamani (VAT)
ambayo ilipitishwa mwaka 2015.
Alisema
kabla ya sheria hiyo wakati inapitishwa vifaa vya ujenzi wa uwanja huo
vilikuwa na msamaha wa kodi lakini baada ya kupitishwa msamahaka huo
uliondolewa hali iliyosababisha baadhi ya vifaa kukwama bandarini na
wakati mwingine kukaa muda mrefu.
Aliongeza
kuwa mradi huo ulikuwa unatarajiwa kukamilika Agosti mwaka jana lakini
ulichelewa kutokana na kuchelewa kuwasilishwa kwa fedha zaidi ya Sh
bilioni 290 kwa ajili ya ujenzi wa awamu ya pili ya mradi huo.
“Tunaiomba
serikali iwezeshe kupatikana kwa fedha za mradi kwa wakati pamoja na
kutatua changamoto zinazojitokeza ili kutochelewesha mradi na kuepuka
gharama zinazoweza kujitokeza kutokana na kuchelewa kukamilika kwake,”
alisema.
Kwa
upande wake, Katibu Mkuu wa Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano,
Dk Leonard Chamuliho alitoa ufafanuzi kuhusu notisi iliyotolewa na
Mhandisi Mshauri ya kusitisha huduma kuanzia jana hadi atakapoliwa deni
lake.
Alisema
tayari serikali inafanyia kazi deni hilo na kwamba ipo katika hatua
nzuri ya kuhakiki vocha za malipo kabla ya kufanya malipo ya mhandisi
huyo.
01.Mwenyekiti
wa kamati ya kudumu ya Bunge ya Maendeleo ya Miundombinu Mhe.Prof
Norman Sigalla akizungumza na wana kamati wakati wa ziara ya mradi wa
ujenzi wa jengo la tatu la abria (terminal) katika kiwanja cha ndege cha
kimataifa Julius Nyerere leo jijjini Dar es Salaam.
02.Katibu
Mkuu wa Uchukuzi Dkt Leonard Chamriho akizungumza wana kamati wakati wa
ziara ya mradi wa ujenzi wa jengo la tatu la abria (terminal) katika
kiwanja cha ndege cha kimataifa Julius Nyerere leo jijjini Dar es
Salaam.
03.Mbunge wa Jimbo la Kwimba,Shanif Mansoor akifafanua jambo leo jijini Dar es Salaam.
Wana
kamati wa kamati ya kudumu ya Bunge ya Maendeleo ya Miundombinu
wakimsikiliza Mwenyekiti wa kamati ya kudumu ya Bunge ya Maendeleo ya
Miundombinu Mhe.Prof Norman Sigalla
.Wana
kamati wa kamati ya kudumu ya Bunge wakitembelea mradi wa ujenzi wa
jengo la tatu la abria (terminal) katika kiwanja cha ndege cha kimataifa
Julius Nyerere leo jijjini Dar es Salaam.
Ujenzi ukiendelea wa jengo la abiria namba tatu (Terminal. )Picha na Emmanuel Massaka,Globu ya Jamii.
Post a Comment